Kuumwa na kichwa kumegawanyika sehemu kuu nyingi sana japo
kuwa 1% yake ni ashirio la matatizo ya kiafya ambayo yame-advance. Kama vile
concussion of brain,meningitis,encephaliti, na stroke. Kuumwa na kichwa pia
inawezatokana na matatizo ya taya, meno au hata kula vitu vya baridi zaidi.
Vyakula vyenye nitrite au monosodium glutamate.
Sehemu ambazo huuma ni kama ifuatavyo:
- Mfumo wa fahamu ambao upo kwenye fuvu la kichwa.
- Baadhi ya neva za fahamu zilizoko usoni
Misuli ya kichwani
Mishipa inayopatikana kwenye fuvu la kichwana chini ya
ubongo kuna mifumo ya fahamu yenye hisia. Kumbuka fuvu na tishu za ubongo kwa
zenyewe haziumi kwani hazina mifumo ya fahamu ambayo inahisia.
Mambo haya 12 nayo yanahusika sana.
1:Nervous tension headaches;
Ni maumivu ya kichwa endelevu upande mmoja au pande zote za
misuli ya shingo na upande wa juu wa mgongo,kuumwa na kichwa pamoja na
kusinzia. Tumia vitamin b2 na c , ounguza au acha matumizi ya
sukari,kahawa,chakula chenye kukusababishia mzio,misongo ya mawazo na ufanye
mazoezi yakutosha.
2: Cluster headaches;
Kichwa kuuma haswa upande mmoja wa kichwa kwa maumivu
makali, machozi humtoka mtu na makamasi kwa mbali. Kitu cha kwanza ni kutumia
chakula chenye protein ya kutosha, epukana na chakula chenye mzio kwako.
3: Hangover headaches;
Hii ni hali ya kichwa kuuma kwa sababu ya matumizi makubwa
ya vinywaji vikali haswa pombe. Weka barafu chini ya kichwa yaani maeneo ya
kichogoni au shingoni,kunywa maji mengi na juice ya matunda freshi na uache
pombe.
4: Exertion headaches;
Hutokea pale ambapo mwili utatumika sana na haswa kwenye
ngono. Weka barafu linalouma, kula mlo kamili na usifanye mazoezi.
5: Caffein headaches;
Hali hii hutokea pale ambapo umeacha matumizi makubwa sana
ya kahawa kwa ghafla. Kunywa kiasi kidogo cha kahawa kuondoa maumivu na
upunguze matumizi kidogokodogo mpaka utakapo acha kabisa.
6: Sinus headaches;
Maumivu haya huanzia upande wa kulia na kushoto wa pua na
kupanda mpaka kichwani. Kula vitamini C kwa wingi na umuone mtaalamu wa afya
maana saa zingine hii utkana na maambukizi.
7: Bilious headaches;
Kichwa na macho huuma haswa kipanda uso na husababishwa na
kula sana, kula vibaya, kutofanya mazoezi na kukosa choo. Fanya mazoezi na
kunywa maji yakutosha na kasha fanya enema.
8: Hunger headaches;
Maumivu ya kichwa ambaya husababishwa na kutokula kwa muda.
Kula chochote ilimradi kiwe ni protein au carbohydrates .
9: Eyes ram headaches
Haya ni maumivu yanayotokea kwenye macho na wengi hudhani
labda wameangalia vibaya japo saa zingine inaweza kuwa sababu. lakini chanzo
chake haswa ni ubongo kufanya kazi kupita kiasi. Badili mtindo wa maisha na
kama ni mtumiaji wa miwani ni vyema ukamuana mtaalamu aangalie kama lensi
zimepotea nuru au la.
10: Menstrual headaches;
Hali hii hutokea kwa kina mama kipindi cha yai kupevuka.
Hutokana na mabadiliko ya hormone, muone mtaalamu wa afya.
11: Arthritis headaches;
Haya ni maumivu ya kichwa yanayosikika mpaka shingoni na saa
zingine mpaka mgongoni ambayo husababisha maumivu haswa unapozidisha mwendo au
shughuli. Kitu kikubwa ni kutibu ugonjwa unaosababisha hali hiyo.
12: Hypertension headaches;
Ni maumivu ya kichwa chote, mwendo mkubwa pia huongeza
maumivu. Hali hii husababishwa na shinikizo la damu. Tibu au pambana kushusha
shinikizo la damu na halii itaisha bila shaka.
Kabla ya kukupa dawa na ushauri wangu nina maswali nikuulize
unijibu.
Je unapata Usingizi wa kutosha? Unalala usiku masaa mangapi?
Je, unakunywa maji ya kutosha? Una miaka mingapi? Unapata haja kubwa ya
kutosha? Nenda pia kapime macho yako na ukapime tena kwenye mishipa yako ya
fahamu huenda una matatizo. Na kitu kingine unakuwa upo juani uwe unavaa
kichwani kofia.



No comments:
Post a Comment