Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, August 21, 2014

DZEKO ASAINI MKATABA MPYA MAN CITY HADI 2018

Edin Dzeko amesaini mkataba mpya wa miaka minne Manchester City
MSHAMBULIAJI Edin Dzeko amesaini Mkataba wa miaka minne na mabingwa wa Ligi Kuu ya England, Manchester City. 
Mwanasioka huyo wa kimataifa wa Bosnia ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter juu ya kusaini kwake mkataba mpya akisema: "Furaha na kujivuniaa kusaini mkataba wangu mpya na Manchester City. Nipo hapa ambako ni kwangu. Nimerefusha hadi 2018,". 

 
Mpachika mabao huyo amefunga 
mara 65 katika mechi 156 alizoichezea klabu hiyo tangu ajiunge nayo kutoka Wolfsburg mwaka 2011. 

No comments:

Post a Comment