Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, August 30, 2014

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO

Chelsea wameanza mazungumzo na mshambuliaji wa QPR Loic Remy, 27, baada ya Fernando Torres, 30, kwenda AC Milan (Telegraph), kiungo wa Manchester United Tom Cleverly, 25, anafikiria kwenda Aston Villa kwa pauni milioni 7, baada ya kuzungumza na nahodha wa zamani wa Man Utd Roy Keane ambaye 
 
sasa ni meneja msaidizi Villa Park (Daily Mirror), meneja mpya wa Crystal Palace Neil Warnock anataka kumchukua beki wa QPR Armand Traore, 24, kwa pauni milioni 2.5 (Sun), Arsenal wamepata matumaini makubwa ya kumchukua winga Alessio Cerci, 27, baada ya rais wa Torino, Urbano Cairo kusema mchezaji huyo atauzwa kwa bei stahiki (Daily Star), Manchester United wanataka kumsajili beki Timothy Fosu Mensah, 16, kutoka Ajax (Daily Express), uhamisho wa beki Marcos Rojo, 24, kwenda Manchester United uko hatarini kutokana na kutopata bado kibali cha kufanya kazi na pia wakala wa tatu wa uhamisho aliyepo kwenye mkataba wake (Sun), West Ham wanakaribia kukamilisha uhamisho wa Alex Song, 26, kutoka Barcelona kwa mkopo (Daily Mail), Birmingham City wanataka kumchukua Hatem Ben Arfa, 27, kutoka Newcastle kwa mkopo (Newcastle Chronicle), Manchester United wanahitaji kutoa pauni milioni 5 zaidi kuweza kumsajili Arturo Vidal kutoka Juventus huku klabu hizo mbili zikiendelea na mazungumzo kabla ya dirisha la usajili kufungwa Jumatatu (Tuttosport), Benfica wanajiandaa kutoa pauni milioni 7.9 kumtaka mshambuliaji wa Arsenal Joel Campbell (O Jogo), Manchester United wamekubali kutoa pauni milioni 14.2 na Ajax kumchukua Daley Blind (De Telegraaf), Chelsea wako tayari kuongeza juhudi kumfuatilia mshambuliaji wa Roma Mattia Destro kufuatia kuondoka kwa Fernando Torres (Daily Mirror). Zimesalia siku mbili kabla ya dirisha la usajili kufungwa Jumatatu. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Cheers!!!!

No comments:

Post a Comment