Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, September 25, 2014

Mmiliki wa Alibaba atajirika zaidi

Mwanzilishi wa mtandao wa Alibaba ndiye tajiri mkubwa zaidi nchini Uchina kulingana na rekodi za kampuni yake.
Hili imethibitishwa na ripoti rasmi ya kifedha ya Hurun.
Bw.Ma ameongoza orodha ya watu tajiri zaidi nchini Uchina kwa mali ya takriban dola bilioni 25 akifuatwa na mwenyekiti wa Wanda Group Wang Jianlin.
Matajiri watano katika ya kumi walio katika orodha


 hiyo, wanamiliki kampuni za mitandaoni huku wakiwabwaga wale wanaomiliki mali isiyohamishika ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiongoza orodha hiyo.
Matajiri nchini Uchina

JINA KAMPUNI
(Thamani Dola za Marekani US$)
1. Jack Ma Yun Alibaba (Teknohama) $25bn
2. Wang Jianlin Wanda ( Uwekezaji, burudani) $24.2bn
3. Li Hejun Hanergy (kawi) $20.8bn
4. Zong Qinghou Wahaha (Vinywaji) $20.8bn
5. Pony Ma Tencent (Teknohama, burudani) $18.1bn
Orodha hiyo inahusisha pia kiongozi wa Tencent Pony Ma.

Mabwenyenye wengine walio katika orodha hiyo ni mwanzilishi mwenza wa mtandao wa intanet marufu sana nchini China Baidu, Robin Li na pia mwanzilishi wa soko la mtandao la JD.com, Richard Liu Qiangdong.

No comments:

Post a Comment