Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, April 6, 2015

Wakazi Mafia wahoji iliko boti iliyozinduliwa na JK


Baadhi ya wakazi wa kisiwa cha Mafia, mkoani Pwani, wamehoji kuhusu kutoonekana kwa boti kubwa na ya kisasa iliyoonyeshwa ikizinduliwa na Rais Jakaya Kikwete, mwaka juzi wakati akizindua gati jipya wilayani humo.
Wakati wa uzinduzi huo wananchi walionyeshwa boti hiyo ya kisasa ambayo waliambiwa ingetumika lakini tangu wakati huo haijaonekana na watu wanendelea kutumia boti zisizo salama.

 
“Tulipoona  boti mpya tukajua  tatizo la usafiri limekwisha lakini mara baada ya uzinduzi wa gati hiyo boti hatukuiona tena hadi leo, tunaendelea kuhangaika na usafiri ambao si salama”, alisema Jumanne Mwinyimvua
Kukosekana usafiri wa uhakika na salama wananchi wa kisiwa hicho wamedai maisha yao yako hatari kwa kukosa usafiri wa uhakika licha ya juhudi zilizofanywa za kujenga gati ambayo haitumiki.
Wamedai wamekuwa wakitumia mitumbwi na boti ndogo ambazo mara nyingi si salama na wakati mwingine huzimika katikati ya maji.
 “Kutokana na ugumu wa usafiri watu wamekuwa wakifa mara kadhaa baada ya boti kupinduka au kuzimika katikakati ya maji  na hatuna mbadala huo ndio usafiri, wakati mwingine uko na familia yake unaomba mungu ufike salama tu maana hakuna jinsi”, alisema  Mwajuma Mohamed mkazi wa Mafia.
Mkazi mwingine wa kisiwa hicho Hussen Omar alisema wanaiomba serikali kufanya jitihada za lazima katika kuhakikisha inaimarisha usafiri katika kisiwa hicho na kuwa viongozi hawaoni kero hiyo kwa kuwa wakienda Mafia hutumia usafiri wa ndege.
Mbali ya ukosefu wa usafiri wa uhakika pia wakazi wa visiwa vidogo vilivyopo ndani ya kisiwa cha Mafia vya Chole, Jibondo, Bwejue na Juani wanakabiliwa na ukosefu wa maji safi na salama kwani maji yaliyoko katika visiwa hivyo ni ya chumvi na kuwalazimu kununua maji kutoka kisiwa kikubwa cha Mafia kwa gharama ya Sh. 1000, kiasi ambacho hawawezi kumudu.
"Usafiri wa kupeleka maji kwenye visiwa hivyo ni wa kukodi mtumbwi au boti kwa gharama ya Sh. 150,000  na wauzaji huuza kwa Sh. 1,000 kwa ndoo moja ya lita 20," alisema mmoja wa wakazi wa Mafia Clever Mwaikambo.
Uchunguzi wa NIPASHE ulibaini kuwa wafanyabiashara wanashindwa kupeleka vyombo vyao vya usafiri kutokana na kukosekana kwa gati upande wa pili wa Nyamisati ambapo boti hunasa kwenye mchanga na hivyo kuharibika na kufanyia matengenezo ya mara kwa mara

No comments:

Post a Comment