Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, November 17, 2015

IDADI YA VIFO VYA WATOTO WACHANGA YAENDELEA KUPUNGUA MBEYA‏


Na Emanuel Madafa,Mbeya

IDADI ya vifo vya watoto wachanga imeendelea kupungua Mkoani mbeya kutoka vifo 602 kwa mwaka 2012 hadi kufikia 568 kwa mwaka 2014  ambapo ni sawa na asilimia 5.7.

Hali hiyo inatokana timu ya uendeshaji wa huduma za afya mkoa kukaa pamoja na kutafuta ufumbuzi wa pamoja na kuweka maazimio ambayo wamekuwa wakiyatekeleza kwa pamoja.

Akizungumza jijini Mbeya mratibu wa huduma za afya ya uzazi na mtoto mkoani humo Ndugu Prisca  Butuyuyu  amesema kutokana na usimamizi huo wameweza kufuatilia  mambo mbalimbali yakiwemo ya upatikanaji wa dawa .

Amesema hatua nyingine iliyofanikisha zoezi hilo ni pamoja na kushughulikia  mapungufu  na changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza katika vituo vya huduma.

Amesema  sanjali na mafanikio hayo pia wanatoa pongezi za dhati kwa shirika la UNICEF  kwa kuendelea kusaidia kutoa fedha za usimamizi  shirikishi katika eneo la huduma za afya na uzazi na mtoto.

 

Butuyuyu amesema kuwa baadhi ya halimashauri  zimeweza kuendesha semina  mbalimbali kuhusu uzazi salama ambazo ni huduma baada ya kujifungua  pamoja na huduma muhimu kwa watoto wachanga.

Hata hivyo  amesema shirika la UNICEF wakishirikiana na KOICA  wamekuja na mpango mwingine wa miaka 4 ya uboreshaji huduma za afya ya uzazi na mtoto.

Mwisho

 JAMIIMOJABLOG

No comments:

Post a Comment