Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, November 18, 2015

KUKAMILIKA KWA DARAJA LA MBWENI JKT LATOA KICHEKO KWA WANANCHI

Daraja lililokuwa linawasumbua mno wakazi na wananchi wa Mbweni JKT, sasa linaelekea mwishoni, hali iliyoanza kuwafurahisha wananchi hao waliokuwa wakisumbuka kuvuka eneo hilo lililokuwa linajaa maji mara kwa mara yanayotoka baharini.

Katika pita pita ya mitandaoni, tuliona picha hizi ambazo tayari zimeshapokewa kwa shangwe kutokana na wananchi hao kuanza kulitumia. Ikumbukwe kwamba kutokuwapo kwa daraja hili kulileta usumbufu mkubwa kwa wananchi. Kabla ya uwapo wa daraja hili, magari yalilazimika kupita kwenye maji na pengine yanapokuwa mengi kushindwa kuvuka. Ni kutokana na daraja hili, shukrani za dhati ziende kwa JKT 


wanaojenga daraja hili, serikali Kuu kwa kupitia Mkuu wa Wilaya Kinondoni, DC Paulo Makonda na watendaji wote waliohakikisha kwamba utengenezaji wa daraja hili unakamilika ili kuondoa adha kwa wakazi na wananchi wa Mbweni JKT.
Mkazi mmoja wa Mbweni aliyeshindwa kutaja jina lake alitumia muda mwingi kuwasifu wahusika kwa kulisimamia vyema daraja hilo litakalokuwa mkombozi kwa wananchi wa eneo hilo na wote wanaoishi jijini Dar es Salaam.


Picha ya daraja hili la Mbweni JKT ilipigwa kwenye gari.

No comments:

Post a Comment