Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, November 18, 2015

BOMOA BOMOA YAFANYIKA ENEO LA MWENGE JIJINI DAR


 Tingatinga likibomoa moja ya nyumba iliyojengwa kwenye hifadhi ya barabara eneo la Mwenge barabara ya TRA leo asubuhi. Wakazi waishio Mwenge waliotakiwa kuondoka na Serikali maeneo hayo kwa kuwa sio sehemu rasmi na nyumba zao kuwa zimewekewa alama ya mkasi wabomolewa nyumba zao,jijini Dar es Salaam. Zoezi hili linaonekana ni muendelezo wa Bomoa bomoa maeneo ambayo yashaakatazwa na ikikumbukwa ni siku chache tu wakazi waliokuwa wanaishi eneo la kidongo chekundu kurasini nao kukumbwa na kadia hii.Picha na Geofrey Adroph wa Pamoja Blog
 Tingatinga likiwa limemaliza kubomoa moja ya nyumna eneo hili la mwenge jijini Dar
 Baadhi ya vyombo pamoja na vifaa mbalimbali vilivyookolewa katika eneo la ubomoaji uliofanyika leo Mwenge eneo la Barabara ya TRA leo asubuhi. Ubomoaji huu umeanza saa kumi za alfajiri na kumalizika saa tatu za asubuhi.

 wananchi wakishuhudia ubomoaji huo ambapo ulinzi uliimarishwa vizuri.
 Hakika ulinzi ulikuwa ni wakutosha wakati wa zoezi la bomoa bomoa lililofanyika leo Eneo la Mwenge barabara ya kwenda TRA
 Hali halisi baada ya tingatinga kubomoa majengo yaliyojengwa kwenye hifadhi ya Barabra
  Wafanyabiashara wakiokoa baadhi ya mali zao kutoka kwenye vifusi vya udongo na mabati baada ya kubomolewa maeneo yao ya biashara leo asubuhi 

Tingatinga likiendelea na kazi

No comments:

Post a Comment