Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard
Membe amempongeza Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli kwa kupiga
marufuku safari za nje ya nchi, akisema mawaziri na watendaji wa
Serikali walikuwa wakigongana angani na ndege utadhani Tanzania ilikuwa
ikiwaka moto.
Mbunge huyo wa zamani wa Mtama alisema uamuzi huo utaokoa fedha nyingi
za Serikali na kumtaka Rais kushusha rungu hilo hadi kwenye mashirika.
Wakati Membe akieleza hayo, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue
alisema kila safari ya nje ina gharama yake na kila safari itakayofutwa
zitapatikana fedha kusaidia masuala mengine ya maendeleo katika jamii.
Juzi, Dk Magufuli alipiga marufuku safari za nje ya nchi kwa watendaji
na kwamba shughuli ambazo wangekwenda kuzifanya, kuanzia sasa zitahitaji
kibali kutoka kwake au zitafanywa na mabalozi wa Tanzania walioko
katika nchi husika.
Jana Membe alisema: ?...Tulikuwa tunagongana huko hewani utadhani huku
nyumbani kunaungua moto. Tunapobaki huku ndani tunaokoa hela nyingi na
nina hakika (Dk Magufuli) ataingilia hata kwenye mashirika. Kuna wakuu
wao wanasafiri kila siku, nina hakika wataguswa katika hili. Lazima
kuziokoa pesa za kufanyia shughuli nyingine mimi naunga mkono mia moja
kwa mia hili.?
Alisema kitendo cha Rais Magufuli kufuta safari za nje hakina maana
kwamba uhusiano wa Tanzania na nchi hizo unakufa. ?Hajakataza wageni,
wafanyabiashara wa dunia wala wawekezaji kuja Tanzania, hata wawekezaji
hawawezi kukataa kuja Tanzania waache gesi, dhahabu, almasi au
tanzanite.?
Alisema wapo watu wanaodhani kuwa kauli ya Rais Magufuli itamhusu hadi
Waziri wa Mambo ya Nje ?... atakwenda nje maana ukishamuita waziri wa
mambo ya nje lazima aende nje. Dk Magufuli hawezi kusema hivyo.
Hutasikia amekatazwa maana ndiyo wizara yenyewe na inashughulika na
dunia.?
Alisema kauli hiyo pia haina maana kwamba Wizara ya Mambo ya Nje
imefutwa kwa kuwa balozi za Tanzania zilizopo nje zipo chini ya wizara
hiyo.
CHANZO: Mwananchi
Dkt Jakaya Kikwete Apongeza Kasi ya Ukuaji Taasisi za Fedha, Aipongeza NBC
Ushirikiano na Wateja.
-
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete ameelezea kuridhishwa
kwake na kasi ya ukuaji pamoja na uimara wa taasisi za fedha hapa nchini
huku akizis...
24 minutes ago
No comments:
Post a Comment