Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, February 11, 2016

TAZAMA PICHA 10::JANGILI ALIYETUNGUA HELKOPTA SEREGENTI HUYU HAPA, MCHEKI NA INTEREJENSIA WA NGORONGORO ALIYERATIBU TUKIO HILO.


  Njile Gonga (28) Huyu ndiye Jangili anadaiwa kutungua helkopta katika pori la Akiba la Maswa lililopo katika Wilaya ya Meatu Mkoani, ambapo katika tukio hilo rubani wa helkopta hiyo Rodgers Gower (37) raia wa uingereza huku Mwenzake Nicholas Beste (43) raia wa Afrika Kusini akinususrika kifo.


Iddy Mashaka (49) ambaye ndiye alikuwa Mkuu wa kitengo cha Interejensia katika hifadhi ya taifa Ngorongoro, ambaye anadaiwa kuwa kiunganishi Mkuu wa kutekeleza tukio la kutunguliwa kwa helkpta hiyo.

Hali ya ulinzi na usalama ilivyokuwa imehimarsihwa mahakamani pamoja na kituo cha polisi Bariadi.


Watuhumiwa wakiwa ndani ya gari la polisi, baada ya kufikishwa kituo cha polisi Bariadi wakitokea wilayani Meatu kwa ajili ya kufikishwa mahakamani.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Elaston Mbwilo akionyeshwa watuhumiwa wa ujangili ambao walihusika kutungua Helkopta.

Iddy Mashaka (49) ambaye ndiye alikuwa Mkuu wa kitengo cha Interejensia katika hifadhi ya taifa Ngorongoro, ambaye anadaiwa kuwa kiunganishi Mkuu wa kutekeleza tukio la kutunguliwa kwa helkpta hiyo.




Watuhumiwa wakiwa Mahakamani.








Watuhumiwa wa tukio la kutungua ndege aina ya Helkopta na kumuua rubani wake Rodgers Gower (37) raia wa uingereza lilitokea mnamo tarehe 29/01/2016 katika pori la akiba Maswa wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu, leo (jana) wamefikishwa mahakani kusomewa mastaka yanayowakabili.




Watuhumiwa hao walifikishwa katika mahakama ya Mkoa wa Simiyu, chini ya ulinzi wa mkali wa askari polisi, huku umati mkubwa wa wananchi wa mji wa bariadi waifurika kushuhudia watuhumiwa hao.

Akiwasomea mashtaka watuhumiwa hao Wakili mwandamizi wa serikali Mkoa wa Simiyu Yamiko Mlekano alisema kuwa washitakiwa wote 9 wanakabiliwa na kesi tatu ambazo ni Uhujumu uchumi, mauaji pamoja na umiliki wa siraha bila ya kibali cha serikali zenye mashtaka tofauti.

Katika kesi ya Uhujumu uchumi iliyosomwa chini ya Hakimu mkazi mfawidhi mwandamizi wa mahakama hiyo John Nkwabi katika shtaka la kwanza mtuhumiwa namba moja Iddy Mashaka (49) anatuhumiwa kujihusisha na kuratibu tukio la uhujumu uchumi kinyume na kifungu 4(1)(d) sura (57) (1) na 60 (2) cha makosa ya uhujumu uchumi sheria namba 200 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Mlekano alisema kuwa katika kosa hilo mshitakiwa kati ya tarehe 6 januari na 1/02/2016 katika wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu aliwashauri Mshitakiwa namba mbili Shija Mjika (38) kuua wanayama wasiyoruhisiwa kama tembo.

Katika shtaka la pili wakili huyo aliwataja watuhumiwa namba mbili hadi tisa ambao ni Shija Mjika (38) Njile Gunga (28), Dotto Pangali (42) Moses Mandagu (48) Dotto Huya (45), Mwigulu Kanga (40) Mapolu Njige (50) pamoja na Mange Barumu (47), watuhumiwa kwa kosa la uhujumu uchumi.

Katika shtaka hilo wakili aliieleza mahakama kuwa kati ya tarehe 21/01/2016 na 29/01/2016 katika wilaya ya Meatu, watuhumiwa hao walipanga na kuratibu tukio la kuwinda wanyama aina ya tembo bila ya kibali cha serikali.
Hata hivyo wakili huyo alieleza kuwa katika shtaka la tatu watuhumiwa
namba mbili hadi tisa waliotajwa hapo mwanzo, watuhumiwa kujihusisha na uwindaji wa wanyama wasiyoruhusiwa kinyume na kifungu 47(a)(aa) cha sheria namba 5 ya mwaka 2009 sambamba na sura 14 (a) na kifungu 57 (1) cha uhujumu uchumi sura 200 iliyofanyiwa marekebisho 2002.

Alisema katika shataka hilo mnamo kati ya tarehe 26/01/2016 na 29/01/2016 katika hifadhi ya Mwiba katika kijiji cha Makao wilayani Meatu watuhumiwa walimuua tembo mwenye dhamani ya shilingi Milion 32,891,100 bila ya kibali cha serikali.

Katika shtaka la nne watuhumiwa namba mbili hadi tisa wanatuhumiwa kwa kosa la kumiliki nyara za serikali kinyume cha sheria namba 86(1)(2)(b) cha uhuwifadhi wa wanyama pori sheria No 5/2009 sambamba na sura ya 14(d) na sura 57(1) cha uhujumu uchumi sura ya 200.

Katika maelezo ya kosa hilo ilidaiwa mahakamani hapo kuwa washtakiwa kati ya 29/01/2016 na tarehe 6/02/2016 katika wilaya ya meatu mkoa wa simiyu walikamatwa na nyara za serikali ambazo ni meno ya tembo yenye uzito wa kilo 31 yenye thamani Milioni 32,891,100 bila ya kibali cha serikali.

Katika shtaka namba tano watuhumiwa namba moja na mbili ambao ni Iddy Mashaka (49) pamoja na Shija Mjika (38) wanatuhumiwa na uuzaji wa nyara za serikali kinyume na kifungu cha sheria 84(1) cha uhuwifadhi wa wanyama pori sheria No 5/2009 sambamba na sura ya 14(b) na sura 57(1) cha uhujumu uchumi sura ya 200.
Katika kosa hilo wakili alisema kuwa kati ya tarehe 6/01/2016 na tarehe 1/02/2016 katika wilaya a Meatu Mkoani Simiyu, watuhumiwa walikamatwa wakiwa wanajihusisha na uuzaji wa nyara za serikali bila ya kibali.

Hata hivyo katika kesi namba mbili ya Mauaji wakili Mlekano aliiambia mahakama kuwa watuhumiwa ambao ni Shija Mjika (38), Njile Gunga (28) Dotto Pangali ( 42) pamoja na Moses Mandago (28) wanashtakiwa kwa kosa la mauaji kinyume che sheria ya 196 na 197 cha kanuni ya adhabu namba 16 iliyofanyiwa mwaka 2002.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa watuhumiwa hao mnamo tarehe 29/01/2016 katika hifadhi ya Mwiba kijiji cha Makao wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu walimuua rubani wa ndege aina ya helkopta rubani wake Rodgers Gower (37) raia wa uingereza.

Katika kesi zote Mbili kwa mujibu wa hakimu huyo alisema kuwa watuhumiwa hawatakiwi kujibu chochote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi hiyo, ambapo keshi hizo zilihairishwa mpaka terehe 24/02/2016 mpaka zitakapotajwa tena.
Sambamba na hayo katika kesi ya tatu ambayo ni kukutwa na siraha kinyume cha sheria na pasipo leseni ilisikilizwa katika mahakama hiyo chini ya Hakimu mfawidhi wa wilaya Bariadi Mary Mrio ambapo watuhumiwa walikabiliwa na mashitaka matano

Watuhumiwa hao ni Mange Buluma,Shija Mjika,Dotto PanganiNjile Ngunga,Moses Mandagu,Dotto Huya na Mwigulu Kanga  ambapo baadhi yao walikiri kumiliki siraha kinyume cha sheria pamoja na riasi akiwemo njile aliyetungua helkopta hiyo.
Watuhumiwa hao ambao Shija Mjika, Moses Mandagu, Njile Ngunga pamoja na Dotto Pangani walikiri mashtaka mawili ambayo ni kukutwa na siraha aina ya bunduki Riffle 303 Namba 06490 kinyume cha sheria pamoja na risasi mbili.

Hata hivyo Njile Ngunga pamoja na Moses Mandagu walikiri pia katika shtaka la tatu, nne pamoja na tano la kukutwa na siraha bila ya kibali, kumiliki risasi bila ya kibali, pamoja na kumiliki tena risasi kinyume cha sheria huku wengine kati ya hao wakikana makosa hayo.

Hata hivyo mahakama haikuweza kutoa hukumu juu ya watuhumiwa hao waliokiri kutokana na vielelezo kutokuwepo mahakamani hapo, ambapo kesi hiyo ilihairishwa mpaka kesho (Leo).

Watuhumiwa wote walirudishwa rumande.

No comments:

Post a Comment