Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, August 8, 2012

TAMASHA LA SIMBA LEO TAIFA ...Simba kuivaa City Stars kwenye tamasha lao



MABINGWA wa Ligi Kuu Tanzania Bara timu ya Simba, inashuka dimbani kuvaana na City Stars ya nKenya katika Tamasha la Simba Day litakalofanyika kesho kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange Kaburu, alisema kuwa maandalizi ya tamasha hilo yanaendelea vizuri kama yalivyopangwa.

Kaburu alisema timu hiyo ambayo imeshika nafasi ya nne katika Ligi Kuu, ilitarajia kuwasili jana jioni kwa ajili ya mchezo huo.

Alisema kuwa katika tamasha hilo milango itaanza kufunguliwa saa 4:00 asubuhi, kutokana na shughuli nyingi zitakazofanyika siku hiyo.

Kaburu alisema katika tamasha hilo wachezaji wa zamani watapewa tuzo maalum kwa ajili ya kuthamini mchango wao.

Alisema kuwa licha ya kupewa tuzo kwa wachezaji wa zamani, pia vyombo mbalimbali vitapata zawadi hizo pamoja na waandishi wake.

Kaburu alisema katika tamasha hilo wachezaji wote waliosajiliwa ambao watacheza katika michuano ya Ligi Kuu na michuano ya Kimataifa ambayo Simba itashiriki watatambulishwa siku hiyo.

No comments:

Post a Comment