Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, November 14, 2012

Bei Za Vyakula Hazishikiki Dar






13th November 2012
Bei za vyakula katika masoko ya jijini Dar es Salaam zimeendelea kuwa juu, huku soko la Kisutu likionekana kuwa kinara wa kuuza bidhaa kwa bei ya juu ukilinganisha na masoko mengine.
Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE jana umebaini kuwa bei za vyakula katika masoko hayo zimekuwa zikipanda kwa kasi kubwa kiasi cha kuzidisha makali ya maisha kwa wakazi wa jiji hilo.
Kinachoshangaza ni kwamba, hata Soko Kuu la Kariakoo, ambalo hapo zamani lilikuwa ni kimbilio la wengi, hivi sasa bei zake ni kali mno.
Hali ni kama hiyo pia kwa masoko ya Temeke, Magomeni, Tandale na Mwanamyamala.
Hata hivyo, bei za bidhaa zinazouzwa katika masoko hayo zimekuwa tofauti zikilinganishwa na zile za katika soko la Kisutu lililopo katikati ya jiji.

No comments:

Post a Comment