Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, February 18, 2013

KAULI YA RIDHIWANI KIKWETE KUHUSU MAAUAJI YA PADRI MUSHI




KAULI JUU YA MAUAJI YA PADRI EVARISTUS MUSHI

Vijana wenzangu na wasomaji wa makala. Hivi karibuni kuna vitendo vimeanz kujijenga katika jamii yetu ambayo haviyoi ishara nzuri tuendako.

Matukio ya kupigwa risasi padri na kuchomwa makanisa na harakati za muamsho. Haya yote pamoja na yaliyotokea geita si mambo ya kufumbiwa macho. Ninaomba niwasihi watanzania wenzangu kuwa haya si mambo yanayoweza kutuimarisha katika umoja na mshikamano wetu. Niwasihi tena kukumbuka kuwa umoja na mshikamano wetu haukuja kama ajali ni misingi ambayo wazee na waasisi wa nchi zetu walikubaliana na kuimarika katika mioyo yao, tusidharau na wala tusibeze.

Mwisho nirudie kuwaomba nikiwakumbusha kauli ya Raisi wetu wa jamhuri ya Muungano kuwa ".... Hivi ni vitendo ambavyo sisi wenyewe tunavipanga. Ni jukumu letu viongozi wa dini,wanaharakati na wanasiasa kukemea haya. Endapo tutaamua kukemea haya kwa vitendo havitaendelea."

Poleni sana waumini wa dini kwa kupoteza kiongozi wenu nami naungana nami katika kuomboleza na NINALAANI kitendo hiki.

No comments:

Post a Comment