Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, June 21, 2013

ISIKE WA BONGO MOVIE APATA AJALI AUMIA KICHWANI,YEYE ADAI KUWA ANACHEZEWA NA WASANII WENZAKE


Isike Samwel
Isike Samwel mwigizaji na mtayarishaji wa filamu Swahiliwood.
MTAYARISHAJI na mwigizaji wa filamu Swahiliwood Isike Samwel akiwa na rafiki yake Dennis David ambaye pia ni mwigizaji wa filamu Bongo walijikuta wakinusurika na ajali mbaya maeneo ya Sinza Afrika sana wakiwa katika gari yake Isike, wakiwa katika barabara inayotokea Polisi mabatini walipoingia barabara ya Afrika sana waligongwa na gari iliyokuwa ikija kwa kasi.

.
Isike Samwel
Isike akiwa na majeraha ya ajali ya gari yake.
Isike akiongea na FC alisema kuwa kabla ya ajali amekuwa akisakamwa na maneno ya vitisho kutoka kwa wasanii wenzake wa Bongo Movie wakimuombea mabaya kwa sababu ya umri wake mdogo wa kufanikiwa kununua gari katika kazi ya filamu na kuwa na mkataba na kampuni moja ya usambazaji, Isike amedai kuwa anamshukru Mungu kuepuka na janga ambalo alilihisi awali.
“Ndugu mwandishi namshukru Mungu kwani hadi sasa dua mbaya zimeniandama kutoka kwa wasanii wenzangu, kwa mfano kuna msanii siwezi kumtaja kwa jina yeye alimfuata rafiki yangu ambaye ni Editor akimwambia mimi ni mwanafunzi wake alafu nimenunua gari nitakufa kama Sharomilionea,”anasema Isike.
.
iSIKE sAMWEL
Isike Samwel akiwa na pozi
Isike Samwel
Isike Samwel akiwa katika pozi la picha.
Msanii huyo amesema toka kununua gari hiyo Vitz mayai imemsababishia maadui ambao ujifanya ni marafiki lakini unapogeuka tu na kuwapa kisogo umsema vibaya na kumuombea mabaya ikiwa ni kumwona akishindwa kumiliki gari na kuliuza na kubaki hana kitu, huku akisema sababu kuu, ni yeye kumiliki gari wakati wasanii wengine wakiwa hawana kitu.
Isike ameusisha ajali yake na imani za kishirikina kwa sababu wasanii wenzake wamekuwa wakimtishia maisha kwa kutumia nguvu za giza












CHANZO FILAMU CENTRAL


No comments:

Post a Comment