Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, August 23, 2013

TAZAMA KWA UMAKINI HIZI PICHA ZA FILAMU MPYA YA MSANII LULU.JE INAWEZA NDO IKAWA CHANZO CHA BASATA KUSEMA IREKEBISHWE?


foolish
Filamu ya Foolish Age ya msanii Lulu.
FILAMU ya Foolish age ya msanii wa kike mwenye mvuto Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ imekwama bodi ya ukaguzi wa filamu na michezo ya kuigiza baada ya kukutwa na picha zilizo nje ya maadili ya Kitanzania, filamu hiyo ambayo ilipanga kuzinduliwa mwezi huu tarehe 30 katika ukumbi wa Mlimani City inahitaji marekebisho chanzo chetu makini kimebaini.

.
Mwigizaji wa filamu Swahilihood Lulu.
Elizabeth Michael
Lulu akiwa katika picha ambayo ndio imekuwa kikwazo katika filamu yake.
Elizabeth Michael
Filamu ya Foolish age ikiwa na picha ambazo zinapigwa na Bodi ya filamu.
Lulu akiwa katika pozi
Elizabeth MichaelKikwazo kilichoikumba filamu hiyo ni nguo fupi zilizotumika katika waigizaji walioshiriki katika filamu hiyo ambayo inatabiriwa kufanya vizuri katika soko la filamu Bongo kama itafanikiwa kuzinduliwa na kuingia sokoni, juhudi zinafanyika kuhakikisha kuwa marekebisho yanafanyika ili kwenda na ratiba kama ilivyopangwa.
Hivi sasa baada ya urasimishaji wa filamu mamlaka na taasisi zinazohusika na masuala ya filamu zimekuwa makini na kuhakikisha kuwa filamu zinazoingia sokoni na zile zinazozinduliwa kukaguliwa kabla ya kufanyika kwa matukio hayo kama ilivyokuwa awali, kama filamu hiyo ya Foolish age itashindwa vigezo vya madaraja yanayotolewa na Bodi hiyo haitaonyeshwa.
Lulu ndio mwigizaji bora wa kike kwa mwaka 2013 kupitia tamasha la filamu la kimataifa la ZIFF katika kipengere cha tuzo za Bongo movie kilichopewa jina la Zuku Bongo movie Awards zilizotolewa katika ukumbi wa Ngome Kongwe.
CHANZO : FILAMU CENTRAL



No comments:

Post a Comment