Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, January 21, 2014

PICHA:::::KIMBUNGA CHALETA UHARIBIFU MKUBWA ENEO LA MBALIZI JIJINI MBEYA

Athari za kimbunga ni kama inavyoonekana eneo la stendi ya Tarafani eneo la Mbalizi wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani Mbeya. Nyumba za watu zaidi ya 40 wamekosa mahali pa kuishi ingawa taarifa zilizopo serikalini zinaonesha idadi ndogo ya walioathirika licha ya maofisa wa serikali kufika eneo la tukio.
Mabati yakiwa juu ya nyaya za umeme eneo la Tarafani mjini Mbalizi Wilaya ya Mbeya Vijijini, majira ya saa saba mchana baada ya kutokea kimbunga eneo hilo ambacho kilianzia eneo la geti la kikosi cha Jeshi la wanancdhi wa Tanzania 44KJ.
Kijana Felix, mkazi wa Mbalizi akiwa katika hospitali teule ya wilaya ya Mbeya,(Ifisi-Mbalizi), akipatiwa matibabu baada ya kujeruhiwa na mabati kichwani yaliyotokana na kimbunga.
 
Katibu tarafa wa tarafa ya Songwe, Felix Lyaniva, akijionea uharibifu wa baadhi ya nyumba za wanancho eneo la Mtakuja Mbalizi, baada ya kuezuliwa na kimbunga.
WATU zaidi ya saba wamejeruhiwa na mapaa ya mabati yaliyoezuliwa na kimbunga kilichotokea eneo la Mbalizi majira ya saa saba mchana, wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani hapa.
Kikosi kzi cha kalulunga media, kilifika eneo la tukio na kujionea hali halisi n kukuta baadhi ya familia zikiwa zimekosa makazi ya kuishi baada ya nyumba zao kuezuliwa mapaa na baadhi ya vitu kutoonekana katia makzi yao.
Maeneo ambayo yameathirika zaidi ni pamoja na eneo la Mtakuja, Chapakazi na Tarafani ambako maduka zaidi ya nane yaliezuliwa na bidhaa kupotea huku vibaka na wakijitwalia mali hizo kwa kupigana kabla na baada ya kufika askari.
Wakati wa tukio hilo, umeme ulileta hitilafu katika kamazi mengi kutokana na upepo mkali kung'oa nyaya katika makazi ya wananchi ambapo watumishi wa Tanesco walifika eneo la tukio na wanatarajia kuanza kufunga umeme huo kesho kwa mujibu wa maafisa wa tanesco waliofika eneo la Tukio.
Muuguzi mkuu wa hospitali teule ya wilaya ya Mbeya, Dr. Sikitu Mbilinyi, alithibitisha kupokea baadhi ya majeruhi katika hospitali hiyo na kuwaruhusu baada ya kuwapatia matibabu.
Wakati huo huo, ajali ya Lori aina ya Volvo, limegonga magari zaidi ya matano eneo la stendi ya Zamani Mbalizi lakini hakuna vifo vlivyotokea katika matukio yote mawili. 
CHANZO kalulungablog

No comments:

Post a Comment