
MAJANGA! Siku chache baada ya hivi karibuni kudaiwa kunywa sumu, staa mkubwa wa sinema Bongo, Wastara Juma amepata tena ajali mbaya.

Akizungumzia tukio hilo kwa masikitiko, Wastara aliliambia gazeti hili kuwa kabla ya kufika kwenye kituo cha kununulia umeme (Luku) alikutana na lori kubwa lililokuwa kwenye mwendo kasi huku likiwa limewasha taa fulu.

Wastara alisema baada ya hapo alikimbizwa katika Hospitali ya TMJ, Dar ambapo alisafishwa majeraha (dressing) kisha akapatiwa matibabu na baadaye aliruhusiwa kurudi nyumbani.
“Nimenusurika kifo, namshukuru sana Mungu kwani ajali ilikuwa mbaya nilihamishwa kwenye siti niliyokuwa nimekaa na kurushwa kwenye siti nyingine huku nikijigonga na kuumia kichwani.

“Namuomba Mungu anisaidie maana naona mambo yanakwenda ndivyo sivyo na kwa nguvu zangu mwenyewe siwezi,”alisema Wastara.
Hata hivyo, Wastara kwa sasa anaendelea vizuri japokuwa bado anaumwa kichwa na mguu.
Wastara ameshapata ajali mara kadhaa ikiwemo ile ya pikipiki aliyopata mwaka 2008 akiwa na aliyekuwa mumewe, Juma Kilowoko ‘Sajuki’ ambapo ilibidi akatwe mguu wa kulia. Pia aliwahi kupata nyingine ya gari akiwa na Sajuki.
Kwa mujibu wa watu wa karibu wa Wastara, kuna watu wanamtakia mabaya ili amfuate Sajuki aliyefariki Januari 2, mwaka jana.
No comments:
Post a Comment