Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, March 6, 2014

MANGULA AONGOZA MAZISHI YA SHEKH TAGALILE IRINGA



 makamu  mwenyekiti wa  CCM Bara  Bw  Philip Mangula  kushoto  akiwa na waombolezaji wengine  katika mazishi ya  shekh Tagalile  leo
Makamu  mwenyekiti  wa  chama cha mapinduzi (CCM) Tanzania  Bara  Bw Philip Mangula ameongoza mamia ya  wakazi  wa mkoa  wa Iringa katika mazishi ya aliyekuwa  shekh mkuu wa  waislam mkoa  wa Iringa Alli Tagalile  aliyefariki  asubuhi ya  leo  katika Hospital ya Rufaa ya  mkoa  wa Iringa.
Mangula  ambae  katika mazishi hayo  alimwakilisha  mwenyekiti wa CCM Taifa  Raid Dr  Jakaya  Kikwete alisema  kuwa  Rais Dr Kikwete  alipenda  kushiriki mazishi hayo ila kutokana namajukumu ameshindwa na kumwagiza yeye  kumwakilisha.
Hata  hivyo  alisema kuwa mwenyekiti  wake Rais Dr  Kikwete  hakuweza  kupata nafasi  ila amesikitishwa  sana na kifo cha Shekh Tagalile na  kuwa Shekh  huyo  atakumbukwa kwa mambo mengi ambayo amepata  kuyafanya  enzi  za uhai wake.
Mangula alisema kwa mambo makubwa aliyoyafanya  marehemu  Tagalile  enzi za uhai wake  iwapo yangeandikwa na kuwekwa katika vitabu  vya kumbu bumbu ni  zaidi ya  kitabu kimoja  ambacho  kingeelezea mambo yake.
 Mwakilishi wa   mufti wa baraza kuu la  Waislam   Tanzania  katika mazishi hayo Shekh  Omary Nzowa alisema  kuwa  mufti mkuu wa Waislam nchini alitegemea  kufika  katika mazishi  hayo ila kutokana na kuwa nje ya nchi  hakuweza  kufika  japo ametuma  salam  zake kwa waislam mkoa  wa Iringa .
Alisema kuwa  Shekh  Tagalile   enzi  za uhai  wake  alikuwa ni mwakilishi  wa Mufti katika mkoa  wa Iringa hivyo  kifo chake  kimeacha pengo kubwa katika mkoa  wa Iringa na nje ya  mkoa.

Hata  hivyo  alisema kuwa baraza la  waislam mkoa wa Iringa  linawapongeza  wakazi wote wa mkoa wa Iringa pamoja na viongozi mbali mbali  wa dini hiyo ya Kiislam na dini  nyingine na  wale  wa  vyama  vya siasa ambao  wamepata  kushiriki akiwemo Bw Mangula.

Shekh  Tagalile  atakumbukwa kwa mchango  wake  mkubwa ambao  aliutoa  enzi za uhai wake  ikiwa ni pamoja na kushirikiana na serikali katika kuwahamasisha  watanzania  kujitokeza katika sense ya  watu na makazi mwaka 2012.
Kwa  upande  wake  mkuu  wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma akielezea  kifo  hicho alisema  kimeacha pengo  kubwa  katika mkoa na  kuwataka viongozi  na  wananchi wa mkoa wa Iringa  kuendelea  kumuenzi kwa mema  yote  aliyotenda .PICHA NA HABARI NA FRANSIS GODWIN

No comments:

Post a Comment