Meneja
wa Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Steven Kazidi
akimnadi Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo Jimbo la
Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete kwa Wananchi wa Kijiji cha
Kibindu,Kata ya Mbwewe,Bagamoyo leo Machi 16,2014.
Mgombea
Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani
Jakaya Kikwete akisalimiana na wanakijiji wa kijiji cha Kwamsanja,wakati
alipofika kwa ajili ya kuzungumza nao na kuwaomba kura katika Uchaguzi
huo.
Mgombea
Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la
Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha
Kwaruhombo,leo Machi 16,2014.Ridhiwani Kikwete ameahidi kuyashughulikia
Matatizo mbali mbali wanayokabiliana nayo Wananchi wote wa Jimbo la
Chalinze,yakiwemo ya Barabara,Maji,Elimu,Matibabu na mengine mengi
ambapo amesema atayafanyia kazi atakapopewa ridhaa ya kuwa kiongozi wa
Wanachalinze.
Mgombea
Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la
Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete (kulia) akimsikiliza kwa makini
Mlemavu wa miguu,Hamis Ibrahim Mkazi wa Kijiji cha Kwarihombo,ambaye
alikuwa akimuomba Mgombea huyo msaada wa kupatiwa Baiskeli ya kulembelea
kutokana na kwamba aliyonayo imechoka sana.Ridhiwani ameahidi
kumpelekea Baiskeli mpya ya kutembelea Mlemavu huyo.
Mgombea
Ubunge kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la
Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete (kushoto) na Meneja wa Kampeni za
Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Steven Kazidi wakiangalia
maendeleo ya ujenzi wa Daraja dogo katika Kijiji cha
Chang'ombe,linalounganisha Barabara inayotoka Kwarihombo kupitia
Kwamsanja mpaka Kibindu,Kata ya Kibindu,ndani ya Jimbo la Chalinze leo
Machi 16,2014.
No comments:
Post a Comment