Katibu
wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda
anayekabiliwa na kesi ya uchochezi katika maeneo mbalimbali mjini
Morogoro na kukaidi amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es
Salaam, akirudishwa rumande baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam
kutupilia mbali maombi yake ya marejeo dhidi ya uamuzi wa Mahakama ya
Hakimu Mkazi Morogoro. Picha na Michael Matemanga
Katibu
wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda amekwaa
kisiki mahakamani baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutupilia
mbali maombi yake ya marejeo dhidi ya uamuzi wa Mahakama ya Hakimu
Mkazi Morogoro.
Sheikh
Ponda anakabiliwa na kesi ya jinai namba 128 ya mwaka 2013 katika
Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, akikabiliwa na mashtaka ya kufanya
uchochezi katika maeneo mbalimbali mjini Morogoro na kukaidi amri ya
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
Sheikh
Ponda kupitia kwa Wakili wake Juma Nassoro aliwasilisha maombi ya
marejeo Mahakama Kuu, baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro
kutupilia mbali maombi yake ya kumfutia shtaka la kukaidi amri ya
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Katika amri hiyo iliyotolewa Mei 9,2013 na Hakimu Mkazi, Viktoria Nongwa, Ponda aliamriwa kulinda amani na kutokutenda kosa lolote kwa kipindi cha miezi 12, baada ya kumtia hatiani katika kesi ya jinai namba 245 ya mwaka 2012,iliyokuwa ikimkabili na wenzake 49.
Katika amri hiyo iliyotolewa Mei 9,2013 na Hakimu Mkazi, Viktoria Nongwa, Ponda aliamriwa kulinda amani na kutokutenda kosa lolote kwa kipindi cha miezi 12, baada ya kumtia hatiani katika kesi ya jinai namba 245 ya mwaka 2012,iliyokuwa ikimkabili na wenzake 49.
Ponda
kupitia kwa wakili wake aliiomba Mahakama hiyo imfutie shtaka hilo
akidai kuwa, mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shtaka hilo.
Mahakama
ya Hakimu Mkazi Morogoro katika uamuzi wake uliotolewa, Oktoba Mosi,
2013, Hakimu Mkazi Richard Kabate anayesikiliza kesi hiyo, alitupilia
mbali maombi hayo alisema mahakama hiyo inayo mamlaka ya kusikiliza
shtaka hilo.
Ni
uamuzi huo uliomsukuma Sheikh Ponda kupitia kwa Wakili wake Nassoro,
kukimbilia Mahakama Kuu akiiomba ifanye marejeo ya uamuzi wa Mahakama ya
Hakimu Mkazi Kisutu.
Hata
hivyo, kinyume cha matarajio yake ya kupata unafuu, badala yake jana
pia alijikuta akiangukia pua katika maombi yake hayo baada ya Mahakama
Kuu kuyatupilia mbali.
Maombi
hayo ya marejeo yalitupiliwa mbali jana na Jaji Augustine Mwarija
aliyekuwa akiyasikiliza baada ya kukubaliana na hoja za pingamizi
lililowekwa na mkurugenzi wa mashtaka.
Akitoa
uamuzi huo, Jaji Mwarija alisema baada ya kusikiliza hoja za pande zote
kuhusiana na pingamizi hilo, anakubaliana na hoja za Wakili wa Serikali
Mkuu, Bernard Kongola maombi hayo yaliwasilishwa mahakamani hapo
kinyume na Sheria.
Jaji
Mwarija alisema kama Wakili Kongola alivyosema, kifungu cha 372 (2),
kilichotumika katika maombi hayo kinazuia maombi ya marejeo ya uamuzi au
amri iliyotolewa na mahakama za chini ambao haumalizi kesi ya jinai.
MWANANCHI
No comments:
Post a Comment