Baadhi
ya Wanakijiji cha Kalenga A,kata ya Kalenga Iringa Vijijini mkoani
Iringa wakiwa wamejitokeza mapema leo asubuhi kupiga kura kumchagua
Mbunge wamtakae wa jimbo hilo la Kalenga.Uchaguzi Mdogo wa Jimbo hilo
unafanyika leo,ambapo vyama Vitatu;CCM,CHADEMA na CHAUSTA vikiwa
vimesimamisha wagombea wake katika uchaguzi huo unaotokana na kifo cha
aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo,pia Waziri wa Fedha,Dk William
Mgimwa.Aidha Wagombea wa Chadema Grace Tendega na wa CCM,Godfrey Mgimwa
ndio wanaopewa nafasi kubwa ya kuchuana na hatimaye mmoja wao kuibuka
kinara kwa kupigiwa kura na Wananchi,huku mgombea wa CHAUSTA,Richard
Minja akipewa nafasi ndogo kutokana na maandalizi hafifu ya ushiriki
wake.
Baadhi
ya akina Mama waliojitokeza kupiga kura mapema leo asubuhi katika
kijiji cha Kalenga A,kata ya Kalenga Iringa Vijijini wakitazama majina
yao kwenye ukuta tayari kwa kutumia haki yao ya msingi ya kumchagua
kiongozi wamtakae kwa kupiga kura
Mmoja
wakazi wa kijiji cha Mangalali,kata ya Ulanda akiwa ndani ya chumba cha
kupigia kura akisubiri kupiga kura mapema leo asubui.
Wakazi
wa kijiji cha Mangalali,kata ya Ulanda jimbo la Kalenga,wakiwa nje ya
chumba cha kupigia kura mapema leo asubuhi.Kwa ujumla katika kata kadhaa
ambako Globu ya Jamii imepita kumekuwepo na utulivu mkubwa,wapiga kura
wamejitokeza kadiri ya uwezo wao bila kubugudhiwa na hali ya namna
yoyote,huku Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa likiwa limejipanga vyema
kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa katika uchaguzi huo Mdogo wa
Ubunge jimbo la Kalenga.
No comments:
Post a Comment