Wanaondoka: Wesley Sneijder (kushoto) akipozi kwenye picha
na mke wake Yolanthe wakati kikosi cha Uholanzi kikijiandaa kwenda Brazil.
WACHEZAJI wa kikosi cha timu ya taifa ya Uholanzi kinachokwenda
kushiriki kombe la dunia 2014 nchini Brazil mwaka huu walionekana wenye
tabasamu kubwa wakati wakijiandaa kupaa angani na ndege licha ya kuagana na
wapenzi wao jana alhamisi.
Nyota hao wa Uholanzi walipozi katika picha na wake na
watoto zao kwenye hoteli ya timu hiyo kabla ya kwenda uwanja wa ndege wa Schipol airport tayari kwa kuanza safari ya
kwenda Brazil.
Wesley Sneijder na Dirk Kuyt walionekana kuwa karibu zaidi
na familia zao huku wakifurahi kwa dakika za mwisho mwisho.
Dirk Kuyt (kushoto) akimuaga mke na mtoto wake.
Mlinda mlango wa Swansea,
Michel Vorm aliungana na kikosi
cha Uholanzi kwenda Brazil
Mtu muhimu: Mashabiki wa Uholanzi wanamtegemea zaidi Robin
van Persie (katikati)
Kila la kheri: Kocha wa Uholanzi Louis van Gaal akiwapungia
mkono mashabiki kabla ya kukwea pipa kuelekea Brazil.
Jamani tunasepa!: Arjen Robben (katikati) akiwasili uwanja
wa ndege wa Schiphol airport uliopo karibu na Amsterdam.
No comments:
Post a Comment