Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, October 18, 2014

Wakili asema Pistorius 'amefilisika'

 Mahakama inayosikiliza kesi dhidi ya mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius imeambiwa kuwa mwanariadha huyo amefilisika.
Hili lesemekana huku pande zote kwenye kesi zikitao akuli yao ya mwisho kabla ya mahakama kutoa hukumu dhidi ya mwanariadha huyo.
Pistorius alipatikana na hatia ya mauji ya mpenzi wake Reeva Steenkamp bila ya kukusudia mwaka jana.
Jaji Thokozile Masipa anatarajiwa kutoa hukumu dhidi ya Pistorius Jumanne.
Anakabiliwa na kifungo cha miaka 15 lakini jaji anaweza kuamua kumpa kifungo cha nje au hata kumtoza faini.
Jaji ataanza kusoma hukumu Jumatatu na upande wa mashitaka unataka Pistorius apewe adhabu kubwa kuambatana na kosa lake.
Lakini mawakili wa Pistorius wameteta wakisema anapaswa kupewa adhabu ndogo kama vile huduma kwa jamii.
Wanadai kuwa mwanariadha huyo huenda akateswa akiwa jela, hoja ambayo imepingwa vikali na mkuu wa magereza.
Pistorius aliangua kilio wakli wake aliposema kuwa pesa zake zimekwisha baada ya kesi yake kufanya kwa mirzi saba.


"sio tu kwamba hana pesa bali anahisi hana tena matumaini,'' alisema wakili wa Pistorius.
Hii ni kesi yake ya kwanza. Nini kimtendekea mwanamume huyu? Nyota yake ilikuwa inaanza kung'ara,'' aliongeza bwana Roux.
Wakili alimuomba jaji kumuonea huruma Pistorius wakati atakapotoa hukumu.
Mnamo siku ya Ijumaa, kiongozi wa mashitaka alikosoa pendekezo la Pistorius kuikabidhi familia ya Reeva pesa. Hata hivyo familia ya Reeva ilikataa pesa hizo ikisema ni pesa za uovu.
Bwana Nel pia alisema ikiwa Pistorius atapewa adhabu ya kiungo cha nje na kuamrishwa kuihudumia jamii, itakuwa ni hujuma kwai adhabu hiyo itakuwa ndogo sana kulingana na kosa lake.chanzo BBC

No comments:

Post a Comment