Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, November 4, 2014

HABARI MBAYA KWA MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED!

Beki wa kimataifa wa Argentina Marcos Rojo ambaye anaitumikia klabu ya Manchester United atakaa nje ya uwanja kwa muda usiopungua wiki 12 ambazo ni sawa na miezi mitatu . Taarifa hii mbaya inakuja baada ya beki huyo kuumia wakati wa mchezo dhidi ya Manchester City uliopigwa jumapili kwenye uwanja wa Etihad ambako United ililala 1-0 . 

Taarifa hii kwa vyovyote itakuwa mwiba mchungu kwa mashabiki wengi wa United ambao hadi sasa wanafahamu fika kuwa timu yao ni mojawapo kati ya timu mbili ambazo zinaongoza kwa orodha ndefu ya wachezaji wenye majeraha yanayowaweka nje ya uwanja.


Hali hii inafanya uchaguzi wa mabeki watakaokuwemo kwneye kikosi cha United kuelekea kwneye mchezo wao dhidi ya Crystal Palce jumamosi ijayo kuwa mgumu hasa ujkizingatia kuwa tayari timu hiyo inamkosa Chris Smalling ambaye atakuwa nje kama adhabu ya ziada baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu , Phil Jones ambaye haijafahamika jeraha la ugoko alilopata litapona lini huku Jonny Evans akiwa karibu kupona lakini hawezi kuwahi mchezo wa jumamosi kwani anahitaji kuwa na utimamu wa mwili thabiti kumfanya aweze kuwa kwneye hali ya kucheza mechi kwa dakika 90.

No comments:

Post a Comment