Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, November 7, 2014

PICHA: AJALI ILIYOUA MAOFISA WA BOT MKOANI MWANZA BAADA YA GARI NA PIKIPIKI KUGONGANA


 MAOFISA wawili wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) waliokuwa wakisafirisha fedha kutoka Mwanza kuelekea Shinyanga, wamefariki dunia baada ya ajali ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali.Chanzo cha ajali hiyo kimeelezwa ni baada ya gari hilo lililokuwa likiongoza msafara wa magari ya BOT kupinduka baada ya kumgonga mwendasha pikipiki.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlowola, alisema ajali hiyo ilitokea jana saa 7:45 mchana katika barabara ya Mwanza - Shinyanga, eneo la Bohari, kata ya Butimba.

 Kamanda Mlowola aliitaja pikipiki iliyosababisha ajali hiyo ni yenye namba za usajili T 792 CTG. "Baada ya pikipiki kuingilia msafara huo, iligongwa na gari la ulinzi lililokuwa kwenye msafara huo aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili SU 3526 mali ya Benki Kuu"


 Kabla ya ajali hiyo, dereva wa gari la ulinzi alijaribu kumkwepa mwendesha bodaboda, lakini kutokana na msafara huo kuwa na mwendo mkali, lilipasuka tairi la mbele na kukosa mwelekeo hivyo kupinduka.

"Pamoja na ajali hiyo, magari yaliyokuwa yamebeba fedha yapo salama, hakuna upotevu wowote wa fedha kwasababu askari waliokuwa kwenye magari mengine walichangamka na kuimarisha ulinzi wakishirikiana na askari wa JWTZ" alisema Kamanda Mlowola.

Kamanda aliwataja waliofariki katika ajali hiyo ni dereva wa gari lililopata ajali Mohamed Mumba na Beatrice Lumelezi ambaye ni Ofisa wa BOT.



" Majeruhi ni watatu ambao kati yao ni askari wawili pamoja na dereva wa bodaboda ambaye nimeelezwa kuwa ana hali mbaya. "Miili ya waliofariki imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando na majeruhi wamelazwa hospitalini hapo kwa matibabi zaidi" alisema.
SOURCE:G SENGO

No comments:

Post a Comment