Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, January 4, 2015

WANAOZALIWA 2015 SINGAPORE KUZAWADIWA

Singapore inaadhimisha miaka hamsini ya taifa hilo mwaka 2015, na serikali ya nchini hiyo inapanga kutoa zawadi maalum kwa kila mtoto atakayezaliwa mwaka huu kuadhimisha ngwe hiyo.
Watoto watakaozaliwa mwaka huu 'watakaribishwa' duniani kwa kupewa kiboksi cha zawadi chenye mahitaji muhimu ambayo wananchi wamependekeza. Kwa mujibu wa tovuti inayoshughulikia mradi huo, zawadi hizo ni pamoja na kumbwewe ya kubebea mtoto, mfuko wa kuwekea nguo za mtoto, na nguo zenye maandishi yasemayo "Mimi ni mtoto wa jubilei ya dhahabu". Wazazi pia watapatiwa kitabu cha 


kuandika matukio muhimu ya kukumbuka, na pia tuzo maalum ya ukumbusho.
Vitu hivyo vilipendekezwa na wananchi mbalimbali, na vina lengo la kuashiria "kila mema kutoka kizazi hiki kwenda kijacho" imekaririwa tovuti hiyo.

Mradi huu ni kwa watoto wote raia wa Singapore watakaozaliwa kuanzia Januari 1 2015, ikiwa ni pamoja na hata wanaozaliwa nje ya nchi lakini ni raia wa Singapore, serikali imesema. Na zawadi huenda zikaongezeka kwa watoto wa mwaka huu nchini humo kwani zawadi zaidi zimeahidiwa na benki kadhaa.

No comments:

Post a Comment