Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, November 15, 2012

KIPINDI CHA 'DIARY YA LADY JAYDEE' KURUSHWA EATV KILA JUMAPILI



 LADY JAYDEE
  Mkurugenzi wa Machozi Band,  Lady Jaydee akizungumza na 
waandishi 
wa habari jijini Dar es Salalaam leo wakati wa uzinduzi wa
 kipindi chake
cha 'Diary Ya Lady Jaydee' kitakachoanza kurushwa hewani kila 
siku ya Jumapili kupitia televisheni ya EATV. Kushoto ni Mkuu wa 
Vipindi EATV, Lydia Igarabuza.

Mkuu wa vipindi wa Televisheni ya EATV, Lydia Karabuza akifafanua jambo wakati wa 
uzinduzi wa kipindi cha televisheni cha 'Diary Ya Lady Jaydee 
kitakachoanza kurushwa hewani kuanzia Jumapili.


DAR ES SALAAM, Tanzania 
Msanii, Lady Jaydee amefanikiwa na kutambulika katika 
kiwanda cha
 muziki ndani na nje ya nchi, huku akitunukiwa tunzo nyingi 
zaidi akiwa
 albamu zake tano. Pamoja na kuwa anaendelea na fani yake ya 
muziki, Lady Jaydee ameamua kuwafikia na kuwaburudisha 
wapenzi wa kazi zake kwa njia nyingine.

Lady Jaydee sasa anaanza sura mpya ya burudani kwa kuleta kipindi 
cha TV kiitwacho DIARY YA LADY JAYDEE, ambacho kutaonekana 
katika kituo cha TV cha EATV

Diary Ya Lady Jaydee itaonesha maisha na hadithi za kweli za Lady 
Jaydee kwa lengo la
Kuburudisha kwa kuonesha mambo yate mazuri anayopitia au
 kuyaona Lady Jaydee
Kuelimisha kwa kushiriki mambo ya kijamii
Kutia moyo wengine wafuate ndoto zao kwa uadilifu
Kuongeza Kipato kama msanii kwa kutangaza biashara 
mbalimbali na hatimae kudumisha ajira binafsi kwa 
njia ya sanaa.

SHUKRANI
Lady Jaydee anatoa shukrani kwa mashabiki kwa kuendelea
 kumpokea, jambo ambalo linampa nguvu zaidi ya kufanya kaza.

pia anashukuru sana vyombo vya habari na zaidi anawashukuru 
EATV na washirika wake kwa kumpa nafasi ya kurusha kipndi 
chake kipya Diary Ya Lady Jaydee.
EATV imekuwa mchango wa aina yake katika kuwakuza 
wasanii Tanzania.

WITO
Lady Jaydee anatoa wito kwa vyombo vya habari kuendelea
kushirikiana na naye kwa kila namna, ili kukuza na kuendeleza
 kipaji chake na sanaa ya muziki wa Tanzania kwa ujumla wake.

Zaidi anatoa wito kwa makampuni kishiriki na kuungana nae 
ili waweze kumpa nguvu msanii, kutangaza biashara zao na 
kushawishi ajira katika fani ya muziki.

Na mwisho Lady Jaydee anawaribisha wote kusikiliza CDs zake 
au kuburidika na kundi lake la Machozi Band au kupata chakula
 ktk mgahawa wake wa kisasa Nyumbani Lounge au ukiwa 
umepumzika nyumbani utazame kipindi chake Diary Ya
 Lady Jaydee ktk EATV

No comments:

Post a Comment