Kamanda wa Polisi kanda Maalum Dar es Salaam DCP Suleiman Kova akiwa maeshikilia baadhi ya vipande vya meno ya Tembo vilivyokamatwa hivi karibuni katika eneo la Kimara Wilaya ya Kinondoni.
Kamanda wa Polisi kanda Maalum Dar es Salaam DCP Suleiman Kova akifafanua kuwa Jeshi la polisi limeweka mikakati ya mpango kazi ikiwa ni pamoja na kushirikiana na vyombo mbalimbali vya ulinzi na usalama pamoja na kikosi cha zimamoto ili kuhakikisha kuna udhibiti wa matukio ya uhalifu au fujo.
Aidha amesema jeshi hilo pia limefanikiwa kukamata bunduki mbili aina tofauti, moja ikiwa ni Shotgun yenye namba AB 44736 na ya pili ni Greener yenye namba 10883 pamoja na risasi 17.