Muda mfupi uliopita spika wa bunge, Anna Makinda amelazimika kusitisha shughuli za bunge mwanzoni tu mwa hotuba ya kambi rasmi ya upinzani iliyokuwa ikisomwa na waziri kivuli wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Joseph Mbilinyi aka Sugu.Kauli kwenye hotuba hiyo
iliyobabisha spika wa bunge asitishe shughuli za leo hadi jioni ilisema, “Tanzania imegeuka chini ya usimamizi wa wizara ya serikali hii ya CCM kuwa taifa linalotoka nyara wanahabari, kuwatesa, kuwangoa kucha na meno, kuwatoboa macho, kuwamwagia tindikali na hata kuwaua.”
Spika amesitisha bunge hilo ili kupata muda wa kuipitia hotuba hiyo kuondoa kauli za uchochezi.
Sikiliza kipande hicho hapa.
Rais Samia aokoa maisha ya mwananchi mwenye Kansa
-
*Na Mwandishi Wetu.*
*Bibi Clotilda Isidory Kokupima, mkazi wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma,
amemtembelea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEM...
1 hour ago

No comments:
Post a Comment