Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, June 18, 2013

UTAJIRI WA KIM KARDASHIAN UMEONGEZEKA MARA DUFU SOMA HAPA.

WATU wengi wanampenda msanii wa filamu, Kim Kardashian. Kuna mambo mengi yanayowafanya watu hao wampende, kwanza ni umbo na sura yake ya kuvutia. Pia ni kutokana na uwezo wake mkubwa katika utendaji wake wa kazi.
Akiwa kwenye kipindi ‘Keeping Up With The Kardashians’ utafurahi, lazima utapata mambo mapya na pia utamaliza siku yako kwa furaha. Hiyo ni kwa kuwa Kim anafahamu kutawala televisheni.
Licha ya televisheni, mwanamke huyo pia ni mkali kwenye mambo ya mitindo. Mbali ya hayo, dada huyo pia hutenga muda wake kwa ajili ya kucheza filamu ambazo zimekuwa zikimpatia tuzo, mara kadhaa amekuwa akitajwa kwenye makundi ya watu wanaowania tuzo mbalimbali.
Aanza kutikisa
Awali Kim alikuwa akifahamika kiasi tu, lakini umaarufu wake ulipanda ghafla mwaka 2007. Jina la Kim lilikua baada ya video yake ya ngono kati yake na Ray J kuonekana. Kampuni ya Vivid Entertainment ndio ilisambaza nakala za video hiyo. Kim aliingia kwenye mzozo mkubwa baada ya kuishtaki kampuni hiyo. Baadaye Kim alilipwa Pauni 5 milioni. Tukio hilo lilimfanya mwanamke huyo afahamike sana.
Baada ya muda kidogo alitikisa kwenye kipindi cha ‘Keeping Up With The Kardashians’.  Kipindi hicho kimemnyanyua dada huyo kwa kiasi kikubwa na kumpa fedha nyingi na analipwa Dola 400,000 kila sura yake inapotokeza kwenye kioo.
Licha ya shoo hiyo, Kim ana vipindi vya  ‘Kourtney And Khloe Take Miami’, ‘Kourtney And Kim Take New York’, ‘Dancing With The Stars’ na ‘Khloe & Lamar’ ambapo analipwa si chini ya dola 100,000 kwa kila kipindi.
Dada huyo ameanzisha kampuni ya nguo ya D-A-S-H kwa kushirikiana na ndugu zake Kourtney na Khloe. Shughuli zote hizo ndio zinamfanya aingize Pauni 40,000 milioni kwa mwaka.
Licha ya mafanikio makubwa kwenye kazi zake, Kim Kardashian amekuwa hana msimamo kwenye mapenzi na amewahi kuolewa mara mbili kisha kuachika.
Alianza kufunga ndoa na Damon Thomas mwaka 2000 na akaachika miaka miwili baadaye. Mwaka 2011 alifunga ndoa na Kris Humphries ambaye ni mchezaji wa mpira wa kikapu, ndoa hiyo ikadumu kwa siku 72 tu.

Vyombo vya habari vilisema Kim alifunga ndoa na kaka huyo kisha akamuacha kwa sababu alitaka umaarufu. Sasa dada huyo ameangukia kwenye mahaba na Kanye West ambaye ameamua kuzaa naye.  

Kim Kardashian na familia yake 
Huku wakiwa chini ya meneja, Momager Kris Jenner, familia nzima ya Kim ina kipato cha Dola 80 milioni kwa mwaka na dada huyo anachangia nusu ya fedha hizo.
Licha ya fedha hizo za familia, Kim amepata Dola 100 milioni kwa kuvunja ndoa yake ya kwanza. Ushirikiano wa Kim na ndugu zake; Kourtney na Khloe katika kazi, unaingiza fedha nyingi. Mwaka 2012 pekee walikusanya Dola 300 milioni.  
Kutokana na kipato kikubwa, Kim amekuwa akinunua magari ya kifahari na hasiti kubadilisha nyumba pale anapohitaji. Hivi karibuni alimnunulia mpenzi wake, Kanye West, gari aina ya Lamborghini katika sherehe yake ya kuzaliwa.

Kim mwenye umri wa miaka 32 ni mtoto wa Robert Kardashian ambaye ni mmoja kati ya wanasheria wanaofahamika. Mama yake ni Kris Kardashian.


No comments:

Post a Comment