Wanawake wawili (mmoja hayupo pichani) wakiondolewa kwa nguvu kwenye mkutano wa waandishi wa habari ambao ulipangwa kufanyika leo mjini Kuala Lumpur. Wanawake hao ni baadhi ya ndugu ‘waliopotea’ katika ndege aina ya Boeing 777 namba
MH370 iliyopotea zaidi ya siku 10
zilizopita ambao wameilaumu serikali ya Malaysia kwa kutowaambia ukweli
na kuwazungusha kuhusu juhudi za kweli kuhusiana na ndugu zao.
Mmoja wa wanafamilia walipotelewa ndugu akiongea kwauchungu na waandishi wa habari kwenye uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur.
Mwanamke
akiondolewa na maofisa usalama wakati alipojaribu kulalamika kwenye
mkutano wa waandishi wa habari katika hoteli ya Sepang mjini Kuala
Lumpur.
Familia ya Wachina waliokuwa na ndugu katika ndege ya Malaysia, wakisindikizwa kutoka kwenye mkutano wa waandishi wa habari.
Moja ya ndege za Jeshi la Maji la Marekani ikitayarishwa kwenda kuisaka ndege ya Malaysia iliyopotea.
Ndege nyingine ya jeshi la Marekani ikisafishwa ili kwenda kuitafuta ndege ya Boeing 777 iliyopotea.
CHANZO: DAILYMAILY
No comments:
Post a Comment