Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, June 3, 2014

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM,KINANA NDANI YA MERERANI,AKUTANA NA WACHIMBAJI WADOGO WADOGO WA MADINI NA KUSIKILZA CHANGAMOTO ZAO

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akioneshwa vipande vya madini aina ya Tanzanite ,katika mgodi wa mchimbaji mzawa wa madini ya Tanzanite Bi.Suzie Didas Kennedy.Katibu Mkuu wa CCM alitembelea migodi ya wachimbaji wadogo wa Mererani na kuzungumza nao juu ya changamoto zinazowakabili na namna ya kuzitatua. Pichani kati anaeshuhudia ni Mbunge wa Jimbo la Simanjiro,Mh.Christopher Ole Sendeka.
 Moja ya jiwe lenye madini kabla ya kufanyiwa mchakato. 
   Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia namna wachimbaji wadogo wanavyotumia mashine kubebea mchanga kutoka kwenye mgodi wa mchimbaji mzawa wa madini ya Tanzanite Bi.Suzie Didas Kennedy.Katibu Mkuu wa CCM alitembelea migodi ya wachimbaji wadogo wa Mererani na kuzungumza nao juu ya changamoto zinazowakabili na namna ya kuzitatua. 
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Mererani ambao aliwaambia vyama vya Upinzania ni sawa na Jogoo kwani hata awike vipi hawezi fungua mlango na kwa sababu vyama hivyo havipo kwa ajili ya maendeleo ya wananchi basi vinaelekea kufa kwani havina sera mpya za kujinadi kwa wananchi. 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Mererani wilaya ya Simanjiro ambao wengi ni wachimbaj wa wadogo wadogo wa madini kwenye mkutano wake wa mwisho baada ya kumaliza ziara ya siku 26 ambapo alitembelea mikoa mitatu ya Tabora, Singida na Manyara.
 Jengo la Kituo cha Afya cha Endiamtu,Mererani Simanjiro,ambapo Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alikwenda kukagua na kujionea ujenzi wake ulipofikia

 
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akitoka kukagua mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Mama na Matoto cha Endiamtu,Mererani wilayani Simanjiro.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu abdulrahman Kinana akikagua mradi wa ujenzi wa tanki la maji litakaloweza kuhudumia watu 25,000 na kutoa  lita 36,000 kwa saa linalojengwa Naisinyai Mererani.
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kijiji cha Landanai,Wilayani Simanjiro
   Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Landanai,Wilayani Simanjiro
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akishiri ujenzi wa Ofisi  ya tawi jipya la CCM la Kandasikira.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipandisha bendera ya Chama Cha Mapinduzi baada ya kuzindua tawi jipya la CCM tawi la Kandasikira.
 Baadhi ya Wazee wa Kimasai wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipofanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kandasikira,Wilayani Simanjiro.
    Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Kandasikira,Wilayani Simanjiro.
    Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana  akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Kandasikira,Wilayani Simanjiro.PICHA ZOTE NA HABRI KWA HISANI YA MICHUZIJR

No comments:

Post a Comment