Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, January 29, 2016

TAZAMA PICHA::::KLABU YA GENK YAMTAMBULISHA RAMSI MBWANA SAMATTA


FLAVIANA MATATA NA MO DEWJI FOUNDATION WAKABIDHI MSAADA WA CHOO S/M MSINUNE, BAGAMOYO

002Meneja Mwendeshaji wa Mo Dewji Foundation, Francesca Tettamanzi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msinune iliyopo Bagamoyo, Pwani. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msinune iliyopo Bagamoyo, Msami Mgoto (kulia). Katikati ni Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation.
005Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation akisaini kitabu cha wageni kwenye ofisi ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msinune iliyopo Bagamoyo, Msami Mgoto (kulia) alipowasili kwenye hafla fupi ya kukabidhi choo kilichojengwa kwa ufadhili wa Mo Dewji Foundation.
006Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation, Meneja Mwendeshaji wa Mo Dewji Foundation, Francesca Tettamanzi wakiwa pamoja na baadhi ya watu walioongozana nao wakielekea kwenye eneo la tukio.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AZUNGUMZA NA BAADHI YA WABUNGE MJINI DODOMA LEO


 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Vunjo, James Mbatia kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Januari 29, 2016.

ZIARA YA WANAFUNZI WA CHUO CHA ULINZI WA TAIFA MAKAO MAKUU YA POLISI


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu akizungumza na Kaimu Mkuu wa Chuo cha ulinzi wa Taifa (NDC) Brigedia Jenerali Jairo Mwaseba wakati wa ziara ya kimafunzo ya wanafunzi wa chuo hicho Makao makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam jana .
Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi, DIGP Abdulrahman Kaniki akimkabidhi zawadi Kaimu Mkuu wa Chuo cha ulinzi wa Taifa (NDC) Brigedia Jenerali Jairo Mwaseba wakati wa ziara ya kimafunzo ya wanafunzi wa chuo hicho Makao makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam jana.DIGP ni mmoja wa Viongozi waliopitia katika chuo hicho.

PROFESA MBARAWA AKAGUA ATHARI ZA BARABARA MORO ; DODOMA.


 Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Morogoro Eng. Dorothy Ntenga akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa namna maji yanavyopiga kingo za daraja la Dumila wakati Waziri huyo akikagua ujenzi wa kingo mpya zinazojengwa kudhibiti mafuriko hayo.
 Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Dodoma Eng. Leornad Chimagu (kulia),akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu athari za mafuriko katika kingo za barabara ya Gairo-Dodoma eneo la Kibaigwa mkoani Dodoma.

SUMAYE AIANGUKIA SERIKALI WANANCHI KUVAMIA SHAMBA LAKE LA EKARI 33 MABWEPANDE JIJINI DAR ES SALAAM


 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akisalimiana na Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye  Dar es Salaam leo asubuhi mara baada ya kuwasili eneo la Mabwepande nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam kuangalia eneo la ekari 33 la Sumaye lililovamiwa na wananchi.
 WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye (wa pili kulia), na mke wake mama Esther (kushoto), wakimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (kulia) eneo la shamba lake la ekari 33 lililopo Mabwepande Manispaa ya Kinondoni lililovamiwa na wananchi walipotembea eneo hilo Dar es Salaam leo asubuhi.

MGODI WA BULYANHULU WATOA ZAIDI YA MILIONI 300 KWA HALMASHAURI YA WILAYA YA NYANG'WALE KAMA USHURU WA HUDUMA

Meneja Mkuu wa Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew akiwa na wafanyakazi wengine wa Bulyanhulu Gold Mine wakikabidhi mfano wa hundi kwa kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Nyang'wale Venance Ngeleuya ,Wengine wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Wilaya ya Nyang’wale Ibrahim Marwa .

Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulu Graham Crew akiteta jambo na mkuu wa idara ya Mahusiano ya Jamii wa Mgodi  huo Sara Terri wakati wa hafla ya kukabidhi hundi.
Madiwani wa halmashauri ya Nyang’wale wakishuhudia makabidhiano ya hundi hiyo.

RAIS DKT. MAGUFULI AWATEUA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA YA MWANZA NA KATAVI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wawili wa mikoa ya Mwanza na Katavi ili kujaza nafasi za Makatibu Tawala wa mikoa hiyo.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema Rais amemteua Kamishna wa Polisi, Clodwing Mtweve kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, ambako anakwenda kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Faisal Issa ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Kabla ya Uteuzi huo, Kamishna Mtweve alikuwa Kamishna wa fedha na Utawala wa Jeshi la Polisi Tanzania.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARY 29, 2016






MAHAKAMA KUU KANDA YA MWANZA YAFUTA KESI YA KUPINGA MATOKEO JIMBO LA TARIME VIJIJINI.

Kulia ni Mwl.Chacha Heche ambae ni Katibu wa Chadema Mkoani Mara akiongea na wanahabari nje ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza.
Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG
Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza jana imeitupilia mbali kesi ya kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Novemba 25 mwaka jana, katika Jimbo la Tarime Vijijini Mkoani Mara, iliyofunguliwa na aliekuwa mgombea ubunge katika jimbo hilo kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Christopher Ryoba Kangoye.

Katika kesi hiyo, wajibu maombi walikuwa ni Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini Mhe.John Heche (Chadema), Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo mtoa maombi alikuwa akiiomba Mahakama kutengua matokeo ya Uchaguzi Mkuu katika Jimbo hilo kwa kuwa haukuwa huru na haki.

SHUJAA RADIO SHOW YAENDELEA KUTISHA ZAIDI 2016,SASA KUSIKIKA ZANZIBAR NA MIKOA YA KUSINI!

Ulimwengu wa burudani kupitia shoo za redio umeendelea kubarikiwa vilivyo na kijana DJ Tee kupitia shoo yake ya kila wiki ijulikanayo kama SHUJAAZ RADIO SHOW. Kuanzia Novemba 2015, SHUJAAZ imekuwa ikipasua mawimbi nchini Tanzania kupitia EAST AFRICA RADIO na kudhihirisha uwezo alio nao DJ Tee na kuleta burudani bora kwa vijana.

Kutokana na vijana wengi kuhitaji kuwa sehemu ya SHUJAAZ na kutopitwa na burudani za DJ Tee, vituo vingine viwili vikubwa vya redio vimeamua kumpa shavu DJ Tee na sasa shoo yake itasikiza vizuri mjini Zanzibar na viunga vyake, pia mikoa ya Kusini.

“Ni furaha kuona wengi wana-appreciate kazi yangu. Vijana tujumuike kwenye ndichi ya Shujaaz tusikie vijana wengine wanafanya nini na sisi tujitume ili tutoboe na kutisha zaidi mwaka huu” Alisema DJ Tee.

MASHA AFUTIWA KESI ILIYOKUWA INAMKABILI

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeifuta kesi ya kutumia lugha ya matusi kwa maofisa wa Jeshi la Polisi iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani nchini, Lawrence Masha (45) ambaye kwa sasa ni kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Wanamauzo 4,760 wapewa elimu ya ujasiriamali na Tigo


Baadhi ya wanamauzo wa kanda ya pwani ya Tigo wakiwa katika picha ya pamoja siku ya mahafali yao ya kuhitimu mafunzo maalum ya ujasiriamali yaliyotolewa na Tigo

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

jitihada za kuwawezesha wafanyakazi wake wa kujitegemea kumudu changamoto mbalimbali za kikazi na kimaisha, Tigo imewapa wafanyakazi hao wapatao 4,767 mafunzo maalum ya ujasiriamali kupitia mpango wake wa mafunzo kazini.

Mpango wa Tigo wa mafunzo kazini kwa wanamauzo wakujitegemea uitwayo Tigo Sales School (TSS) ulianzishwa mwaka 2012 ambapo kwa mujibu wa Meneja wa TSS Justine Kwizera, kampuni inatarajia kutoa mafunzo hayo kwa wanamauzo wake wote wapatao 10,000 katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.

MTEJA AILALAMIKIA TANESCO CHARAMBE KWA KUCHELEWA KUMUWEKEA UMEME

Mteja Ambwene Kyoga


Dotto Mwaibale

SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco) Wilaya ya Charambe Temeke jijini Dar es Salaam limelalamikiwa na mteja wake mmoja kwa kushindwa kumfungia umeme kwa wakati licha ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Mhongo kuagiza wateja wapya kufungiwa umeme katika kipindi kifupi.

Malalamiko hayo yametolewa na mteja wa shirika hilo Ambwene Kyoga ambaye amelipa sh. 320,960 kwa ajili ya kuwekewa umeme na kupatiwa lisiti namba TDB 16841 kwa ajili ya nyumba yake iliyopo Mbagala Kuu Bucha.

Moto wateketeza bweni la Shule ya Sekondari Edward Lowassa

Bweni la wanafunzi katika shule ya sekondari ya Edwaed Lowassa iliyoko wilayani Monduli mkoani Arusha limeteketea kwa moto na wanafunzi zaidi ya 70 wa kidato cha kwanza wamelazimika kupewa likizo ya wiki moja baada ya kukumbwa na hofu iliyotokana na moto huo.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Bw Salum Selemani amesema moto huo ambao umetekeza mali zote za wanafunzi na majengo unaodaiwa kusababishwa na hitilafu ya umeme za ulianza saa nne usiku wakati wanafunzi wakiwa darsani na hakuna aliyejeruhiwa japo baadhi yao walikumbwa na hofu iliyosababisha wapoteze fahamu na kukimbizwa hosipitali.

IDRIS AKUBALI YEYE NDIYE ALIYEMPA MIMBA WEMA SEPETU,WEMA ANENA SOMA KILA KITU HAPA

Wema alimwambia idris kuwa anataka kusafisha kizazi...idris akasema subiri kwanza tujaribu tuone kwa hiyo akamwambia siku ya kufanya hilo tendo asile kitu chochote kuanzia saa tano na mida ya jioni waweze kufanya kitu hicho..baada ya kufanya hicho kitu  kesho yake wema akaanza kutest mkojo