Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, March 7, 2016

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AMUAPISHA MHE. BALOZI ENG. JOHN WILLIAM KIJAZI KUWA KATIBU MKUU KIONGOZI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi Eng. John William Herbert Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu jijini Dar es Salaam. Balozi Kijazi anachukua nafasi ya Balozi Ombeni Sefue ambaye atapangiwa kazi nyingine.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Eng. John William Herbert Kijazi wakwanza kushoto na Wamwisho kulia ni aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue. 

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA BALOZI WA CONGO NCHI TANZANIA LEO.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Balozi wa Congo Nchini Tanzania Mhe. Mutamba Jean Pierne, wakati Balozi huyo alipomtembelea Makamu wa Rais Ofisini Kwake Ikulu Dar es salaam leo March 07, 2016.

BASATA YAWAPONGEZA LULU NA RICHIE KUSHINDA TUZO ZA AMVCA 2016



Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kama msimamizi na mratibu wa sekta ya Sanaa nchini linapenda kutoa pongezi za dhati kwa Wasanii Single Mtambalike (Rich Rich) na Elizabeth Michael (Lulu) kwa kushinda tuzo za African Magic Viewers’ Choice Awards (AMVCA2016) zilizotolewa mwishoni mwa wiki nchini Nigeria na kushuhudiwa na Dunia kupitia luninga na mitandao ya kijamii.

Katika tuzo hizo Msanii Singo Mtambalike ameshinda tuzo ya Filamu Bora ya Lugha ya Asili (Best Local Language – Swahili) kupitia filamu ya ‘Kitendawali’ huku Msanii Elizabeth Michael (Lulu) akishinda tuzo ya Filamu Bora ya Afrika Mashariki (Best Movie -Eastern Africa) kupitia filamu yake ya ‘Mapenzi’

WASIFU WA KATIBU MKUU KIONGOZI BALOZI MHANDISI JOHN WILLIAM KIJAZI HUU HAPA



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Balozi Mhandisi John William Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi tarehe 6 Machi 2016, akichukua nafasi ya Balozi Ombeni Sefue.

Kabla ya uteuzi huo, Balozi Mhandisi Kijazi alikuwa mwakilishi wa Tanzania nchini India, Singapore, Sri Lanka, Bangladesh na Nepal mwenye makazi yake jijini New Delhi, India kuanzia mwaka 2007 na hivyo kumfanya kuwa Mkuu wa Mabalozi wote wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi.

Vilevile, hadi uteuzi wake, Balozi Kijazi amekuwa Mkuu wa Mabalozi wa Afrika nchini India ambaye amekuwa mtetezi mkuu wa wanafunzi wenye asili ya Kiafrika nchini India.

AUDIO: BAADA YA MUITALIANO KUWAPA TUHUMA NZITO JANUARY NA MWAMVITA MAKAMBA, WAFUNGUKA KUJIBU TUHUMA HIZO

Hatimaye Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira na Muungano), January Makamba na mdogo wake Mwamvita Makamba wamejibu tuhuma za kupokea rushwa kutoka kwa raia wa Italia, Vincenzo Cozzolino ili wamsaidie kupata zabuni ya ujenzi kupata ujenzi wa bandari ya Bagamoyo.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MARCH 07, 2016







MTAZAME RAIS MAGUFULI AKIMTANGAZA KATIBU MKUU MPYA IKULU JIJINI DAR

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amemtangaza katibu mkuu kiongozi mpya kwenye serikali yake ambaye anachukua nafasi hiyo iliyokua kwa Ombeni Sefue, katibu mkuu mpya amekua akifanya kazi kama Balozi wa Tanzania India, mtazame Rais Magufuli hapa chini.

BAADA YA MECHI YA SIMBA NA MBEYA CITY HUU NDIO MSIMAMO WA LIGI KUU YA TANZANIA BARA


MSIMAMO WA LIGI KUU UINGEREZA BAADA YA MECHI ZA JANA


RAIS WA VIETNAM KUFANYA ZIARA YA KWANZA YA KITAIFA NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Augustine Mahiga (Mb.) (kulia), akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu ziara ya kitaifa ya siku 4 ya Rais wa Vietnam nchini, Mhe.Truong Tan Seng kuanzia tarehe 08 hadi 11 Machi, 2016. Ziara hiyo itakuwa ni ziara ya kwanza ya kuja Tanzania pia Afrika. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga naye akisikiliza kwa makini mazungumzo ya Waziri na Waandishi wa Habari.

Waandishi wa Habari wakimsikiliza kwa makini Balozi Mahiga (hayupo pichani). 
Bi. Mindi Kasiga naye akitolea ufafanuzi ratiba nzima ya ziara ya Rais huyo wa Vietnam.

WWF KUSAIDIA UJENZI WA MAJIKO SANIFU KATIKA SHULE TATU ZA MANISPAA YA MOSHI NA KUWEKA SOLAR KATIKA ZAHANATI YA MSARANGA

Shule ya Sekondari , J.K Nyerere iliyopo manispaa ya Moshi ni moja kati ya shule zitakazonufaika na msaada wa kujengewa majiko sanifu na Shirika la kimataifa la Mazingira (WWF-Tanzania) 
Mratibu wa Nishati wa Shirika la kimataifa la utunzaji Mazingira ,(WWF-Tanzania) Dkt Teresia Olemwako akiongozana na wa wakuu wa idara katika Halmashauri ya Manispaa ya Moshi walipotembelea shule ya sekondari J.K Nyerere .

WAZIRI MKUU, KASSIM MAJALIWA AENDELEA NA ZIARA MKOANI SIMIYU

Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akikagua jengo la matibabu ya wazee baada ya kulizindua kwenye hospitali ya Wilaya ya Meatu iliyopo Mwanhuzi akiwa katika ziara ya mkoa wa Simiyu Machi 5, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na watumishi wa serikali katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Metu akiwa katika ziara ya mkoa wa Simiyu Machi 5, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wananchi wakati alipoingia kwenye uwanja wa Stendi ya Mwanhuzi wilayani Meatu kuhutubia Mkutano wa hadhara Machi 5, 2016. 

DKT. SHEIN AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KWENYE MAZISHI YA MZEE HAMID AMEIR MUASISI WA MAPINDUZI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) pamoja na Viongozi wengine na wananchi wakibeba jeneza la Marehemu Mzee Hamid Ameir Muasisi wa Mapinduzi,pia Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa CCM baada ya kuswaliwa wakati wa Mazishi yake yaliyofanyika Kijijini kwao Donge wilaya ya Kaskazini B.Unguja.
Wananchi waliohudhuria katika mazishi ya Marehemu Mzee Hamid Ameir Muasisi wa Mapinduzi,pia Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa CCM wakilibeba jeneza wakati wa Mazishi yake yaliyofanyika jana Kijijini kwao Donge wilaya ya Kaskazini B.Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) pamoja na wananchi na Viongozi wakiwa katika maziko ya Marehemu Mzee Hamid Ameir Muasisi wa Mapinduzi,pia Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa CCM aliyezikwa leo Kijijini kwao Donge wilaya ya Kaskazini B.Unguja. 

MWIGULU NCHEMBA AJIPANGA KUBORESHA UZALISHAJI SHAMBA LA KITULO.

Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mh.Mwigulu Nchemba akiwa na Mbunge wa Makete Mh.Noramn Sigalla wakati alipowasili kwenye shamba la Kitulo ambalo ni moja ya Mashamba makubwa ya kufuga Ng’ombe wa kisasa aina ya Mitamba.
Huwa ni mfano wa Ng’ombe wa kisasa aina ya Mitamba wanaopatikana shamba la kitulo wenye uwezo wa kutoa maziwa lita 15 hadi 20 wanapokamuliwa mara moja kwa kila mmoja.

SERIKALI IPO KWENYE HATUA ZA MWISHO ZA KUANZA UJENZI WA BARABARA YA TANGA,PANGANI

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akionyeshwa eneo la uwanja wa ndege itakakopita barabara ya Mchepuko itakayotoka Horohoro kuunga na inayokwenda Pangani kupitia Utofu, Majani Mapana hadi Duga.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akikagua eneo ambalo barabara ya Mchepuko itakayotoka Horohoro kuunga na inayokwenda Pangani kupitia Utofu, Majani Mapana hadi Duga.

Maonesho ya Siku ya Wanawake Duniani katika Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Kisonge Zanzibar.


Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Maonesho ya Siku ya Wanawake Duniani katika Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Kisonge Zanzibar. katika Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Zanzibar michezani Kisonge akiongozana na Mwenyekiti wa Tanzania Informal Sector Foundation Ndg Masaud Maftah, katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa Maonesho ya Wajasiriamali wa Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akizungumza na Mwenyekiti wa Tanzania Informal Sector Foundation Ndg Masaud Maftaha na  Mwenyekiti wa Zanzibar Informal Sector Foundali Bi Nuru Mohammed Ahmeid, wakati wa hafla hiyo ya Maonesho ya Biashara za Wajasiriamali Wanawake Zanzibar katika maonesho ya Siku ya Wanawake Duniani.

DC -PAUL MAKONDA AZINDUA VITAMBULISHO VYA WALIMU KUPANDA DALADALA BURE JIJINI DAR ES SALAAM


 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (kulia), akimvika kitambulisho Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Turiani, Beatrice Mhina Dar es Salaam i, baada ya kuvizindua vitambulisho hivyo vitakavyotumiwa na walimu kupanda daladala bure wakati wa kwenda kazini kufuatia mpango aliouanzisha wiki iliyopita wa kuwasaidia walimu hao.
DC Makonda akimfika kitambulisho Mwalimu Gideon Mwenenyi.
DC Makonda akimvika kitambulisho, Mwalimu Ramadhani Korowelle.

MAMLAKA YA HALI YA HEWA YATOA TAHADHARI JUU YA MWELEKEO WA HALI YA MVUA NCHINI

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini TMA Dkt.Agness Kijazi (Katikati) akitoa taarifa ya Mwelekeo wa hali ya Mvua nchini kwa kipindi cha mwezi machi hadi mwezi Mei, 2016. Kushoto ni Samwel Mbuya ambae ni Meneja Kitengo Kikuu cha Habari TMA Dar es salaam na Kulia ni Dkt.Hamza Kabelwa ambae ni Mkurugenzi Huduma za Utabiri TMA.
Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG
Mamla ka ya Hali ya Hewa nchini TMA imewatahadharisha Wananchi pamoja na Taasisi mbalimbali ikiwemo za Uokoaji, kujiandaa juu ya namna ya kukabiriana na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua za masika ambazo tayari zimeanza kunyesha hapa nchini.

Mkurugenzi wa mamlaka hiyo Dkt.Agness Kijazi alitoa tahadhari hiyo juzi Jijini Mwanza, wakati akitoa taarifa ya mwelekeo wa Mvua za Masika kwa Kipindi cha kuanzia mwezi Machi hadi mwezi Mei Mwaka huu.

Dkt.Kijazi alisema kuwa mvua za Masika zinatarajiwa kuanza katika wiki ya kwanza nay a pili ya mwezi machi mwaka huu, katika maeneo ya Ukanda wa Ziwa na kusambaa katika maeneo mengine yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee naWatoto, Mh. Dk Hamisi Kigwangala aongoza Matembezi ya " KUTOA AHADI YA UWIANO SAWA WA KIJINSIA "‏

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee naWatoto, Mh. Hamisi Kigwangala akijiandaa kuanza matembezi ya shamrashamra za kuelekea  siku ya wanawake dunia Tarehe 8 Machi  yaliyofanyika jijini Dar es Salaam  . Matembezi hayo yaliyoandaliwa na  Taasisi ya Tanzania women of Achievement(TWA) yenye kauli mbiu ya Kutoa uwiano sawa kijinsia.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee naWatoto, Mh. Hamisi Kigwangala akiwa sambamba na washiriki wa matembezi ya shamrashamra za kuelekea  siku ya wanawake dunia Tarehe 8 Machi  yaliyofanyika jijini Dar es Salaam  . Matembezi hayo yaliyoandaliwa na  Taasisi ya Tanzania women of Achievement(TWA) yenye kauli mbiu ya Kutoa uwiano sawa kijinsia.