Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, June 27, 2012

Matukio mbali mbali hospitali ya Muhimbili leo wakati Dk Steven Ulimboka alipofikishwa

Madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam wakimpakia kwenye Gari Daktari Mwenzao aliepatwa na Mkasa wa Kutekwa Nyara na watu wasiojulikana na ambao walimjeruhi vibaya sana,Dk. Steven Ulimboka aliepatwa na mkasa huo usiku wa kuamkia leo huko katika msitu wa Mabwepande,jijini Dar
Wanahabari wakihangaika kupata picha ya Dk. Steven Ulimboka alieinginzwa kwenye gari hiyo tayari kwa kupelekwa kwenye Taasisi ya Mifupa (MOI) kwa matibabu zaidi.
Madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakiisukuma gari iliyokuwa imempaki Dk. Stevan Ulimboka.
Madaktari na Wauguzi wa Muhimbili wakiwa wamesimama huku wakizungumzia hali iliyompaka mwenzao.

Wanahabari wakitafuta taswira.
hakuna kazi iliyokuwa ikifanyika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakati Dk. Ulimboka akifikishwa hospitalini hapo.









                                                          

VIKOSI VYA URENO NA HISPANIA

Nani

 

 

 

 

 

 

Portugal v Spain - teams



Striker Alvaro Negredo was surprisingly brought into Spain's team for the Uefa Euro 2012™ semifinal against Portugal ((1845 GMT) with coach Vicente Del Bosque leaving out midfielder Cesc Fabregas. Live on SS3, SSHD, Maximo and SuperSport.com


Portugal have been forced to make the first change to their starting lineup at the finals due to striker Helder Postiga's thigh injury and, as expected, Hugo Almeida replaces him in a three-pronged attack with Nani and Cristiano Ronaldo.
Del Bosque's move means Spain will play with a recognised striker after beating France 2-0 in their quarterfinal with a six-man midfield but there is no place for Fernando Torres who is on the bench along with fellow forward Fernando Llorente.
Sevilla striker Negredo, who was thought to be behind both of those strikers in the pecking order, has scored six goals in 11 games for Spain but has appeared just once in the tournament so far - as an 89th minute substitute against Croatia.
Teams
Portugal: 12-Rui Patricio; 21-Joao Pereira, 2-Bruno Alves, 3-Pepe, 5-Fabio Coentrao; 16-Raul Meireles, 4-Miguel Veloso, 8-Joao Moutinho; 17-Nani, 9-Hugo Almeida, 7-Cristiano Ronaldo
Spain: 1-Iker Casillas; 17-Alvaro Arbeloa, 15-Sergio Ramos, 3-Gerard Pique, 18-Jordi Alba; 16-Sergio Busquets, 14-Xabi Alonso; 8-Xavi, 6-Andres Iniesta, 21-David Silva; 11-Alvaro Negredo
Referee: Cuneyt Cakir (Turkey)

HUYU NDIO MCHEZAJI WA UGANDA ALIYEFIA KWENYE MECHI.

Hapa ilikua ni muda mfupi kabla ya kukimbizwa hospitali kabla hajafariki.
Mashabiki wa mpira wa miguu huko Sironko Uganda wamepata mshituko baada ya mchezaji kuzimia kwenye uwanja wa mpira na kufariki dunia wakati akipelekwa hospitali.
Simon Musika ana umri wa miaka 30 na alicheza kwenye hiyo mechi ya timu za mitaani kwa dakika 15 kabla ya kuzimia na kufariki dunia ambapo baada ya taarifa za kifo chake ilibidi mechi isimamishwe.
Ndugu wa marehemu walikusanyika kwenye uwanja wa mpira muda mfupi tu baada ya kifo cha mchezaji huyo.
                                        SOURCE MILLARD AYO

WANAFUNZI WATANO WAFARIKI NCHINI UGANDA BAADA YA MABWENI KUUNGUA MOTO.

 

Wanafunzi watano wameteketea kwa kuungua kwa moto nchini Uganda baada ya moto kuunguza mabweni mawili ya Leos Junior Academy katika manispaa ya Masaka.
Wanafunzi wote waliofariki ni wa elimu ya msingi ambao wameungua hadi kutotambulika, na miili yao imepelekwa katika hospitali ya rufaa ya Masaka.
Kamanda wa Polisi wa Kanda ya Kusini Simon Peter Wafana amesema tayari polisi nchini humo imeanzisha uchunguzi wa chanzo cha moto huo.
Hii ni mara ya pili moto kuzuka katika shule hiyo katika kipindi cha miaka miwili.

BREAKING NUUUUUZ: KOVA AZUNGUMZIA UTEKAJI WA DK. STEVEN ULIMBOKA



 Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamanda Suleiman Kova akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio la utekaji nyara na kujeruhi lililompata kiongozi mgomo wa Madaktari Steven Ulimboka anayedaiwa kutekwa na watu watano wakati akipata kinwaji katika klabu ya Leaders Kiondoni jijini Dar es salaam.

Kamanda Kova amesema Ulimboka aliokotwa na msamaria mwema ambaye hakutaka kumtaja jina lake kiusalama na kutoharibu upelelezo kuwa msamaria mwema huyo alimuokota Ulimboka katika msitu wa Mabwepande na kutoa taarifa kituo cha polisi cha Bunju, ambapo polisi aliyekuwa zamu alichukua maelezo yake na baadae Steven Ulimboka kuletwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Kamanda Kova amesema jeshi la Polisi Kanda Maalum limeunda jopo maalum kwa ajili ya uchunguzi na upelelezi wa tukio hilo la utekaji nyara, kwani ni tukio la kwanza kutoke nchini, ameongeza kwamba wahusika wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo wachukuliwa hatua za kisheria na sheria itafuata mkondo wake ili kukomesha matukio mengine kama hayo
 Waandishi wa habari waimsikilza kamanda Suleiman Kova katika kituo kikuu cha polisi Kati jijini Dar es salaam leo mchana.
SOURCE:FULLSHANGWE BLOG

3000 kukosa udahili vyuo vikuu

 
TUME ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), imesema kuwa wanafunzi 3000 kati ya 40,000
waliomba kujiunga na vyuo mbalimbali nchini wamekosa udahili kutokana na
kasoro mbalimbali.

Katibu Mtendaji wa TCU Profesa Sifuni Mchome, aliliambia gazeti hili kuwa
wanafunzi 37,000 ndio waliofanya maombi hayo kwa usahihi kupitia mfumo
unaojulikana kama 'Central Admission System', udahili wao una makosa
mbalimbali.

“Jana (juzi) niliangalia na kuona wanafunzi 40,000 ndio wamefanya maombi,
hao 3000 ndio wenye makosa mbalimbali, wengine wameingia tu na kufikiri
ndiyo wameshafanya maombi na makosa mengine kama hayo,” alisema Profesa
Mchome na kuongeza: “Barua pepe ambazo zitakuwa zimewarudia ni vyema
wakazifanyia kazi kabla ya siku ya mwisho ambayo ni Juni 30.”

Alisema kuwa Julai 6 TCU itakutana na vyuo ili kupitia majina ya waombaji
ambapo Julai 15 watakaa na kufanya udahili kamili kwa kuwapangia wenye sifa
kwenye vyuo walivyoomba. “Nawaambia wanafunzi wasubiri huo udahili wa Julai
15,” alisema Profesa Mchome.

Katika hatua nyingine, wakuu wa vyuo na wadau wengine wa vyuo vikuu,
walikutana jana jijini Dar es Salaam kujadili mfumo wa pamoja wa tuzo
(University Qualification Framework). Akizungumza wakati wa ufunguzi wa
mkutano wa kujadili mfumo huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu
Selestine Gesimba, alisema mfumo huo utasaidia kuweka viwango sawa vya
mafunzo yanayotolewa na vyuo vikuu vyote nchini.

Katika hatua nyingine, Profesa Mchome alizungumzia wizi uliotokea katika
ofisi hiyo usiku wa kuamkia juzi akisema kuwa, mali zilizopotea ni kompyuta
10 huku thamani yake ikiwa haijajulikana.

Chanzo: Mwananchi

Mtambue mtu aliye nyuma ya mafanikio ya Diamond!




Ulishajiuliza kwanini Diamond yuko smart sana kwa namna anavyozipeleka issue zake za muziki? Hushangai iweje msaniii huyu ambaye wengi walitegemea awe na elimu ya chuo kikuu ndio aweze kuufanya muziki kwa umaridadi mkubwa kiasi cha kutochuja kwa show zake japo zinajipanga kama mayai kwenye tray!
Well, wengi hili wanaweza kuwa wanalijua juu juu tu ama hawalijui kabisa kuwa the person behind Diamond’s music creativity is none other than Ruge Mutahaba!!
Yeah, habari ndio hiyo, hate it or love it.
Tangu show ya aina yake ya Diamonds Are Forever iliyowapa mkwanja mnene wa kuweka benki na kula bata, show ya Dar Live iliyompa sifa Diamond kwa kutua kwenye ‘Uwanja huo wa taifa wa burudani mpaka show ya Big Brother Stargame aliyoifanya mwaka huu. He (Ruge) was the mastermind!
Ameweza kumtengeneza Diamond kuwa bidhaa ya thamani isiyochuja.Hautakosea ukimwita Russell Simmons wa Tanzania. Kwa uzoefu alionao kupitia show zinazoandaliwa na kituo cha Clouds Fm, ameweza kuzijua ramani zote za kupitia ili kufanikiwa ‘kibiashara’ kwenye muziki wa Tanzania. He has the music map in the palm of his hands and never missed a shot!
Kuna mtu mmoja wa karibu sana na Diamond hivi karibuni ametuambia kuwa maandalizi ya show ya ‘Diamonds Are Forever ya pale Mlimani City yalichukua takribani wiki nzima. Ruge alikuwa akienda kila siku kuangalia maendeleo ya rehearsal and he was like, “mmh mmh! Hapo bado,ongezeni nguvu zaidi.”
Kwenye show ya hivi karibuni ya Miss Redds Tanzania huko Arusha, Ruge alionekana kwenye picha akimwelekeza Diamond namna ya kupiga kinanda na ngoma. Haijalishi kama anajua kupiga hivyo vitu ama la,hilo si suala letu, cha msingi ni kuwa ushauri wake unafanya kazi kwa Diamond.
And tell you what, hakuna mtu mwenye connection ya masuala ya muziki iwe ndani ya nchi ama nje kama Ruge! Hivyo kuchuja kwa Diamond katika ramani ya muziki wa kibiashara bado sana.

ANGALIA JINSI MWANAMKE ALIVYOCHOMWA MOTO NA BOYFRIEND WAKE WA ZAMANI{DJ SEK}

Gazeti la Italia lamfananisha Balotelli na ‘King Kong’



MARIO BALOTELLI amejikuta katika kasheshe jingine la ubaguzi wa rangi baada ya gazeti la michezo linalouza na kusomwa zaidi nchini Italia kumfananisha na KING KONG (Gorilla).
Gazeti hilo la asubuhi ‘Gazzetta dello Sport’ lilichora picha ya Balotelli akiwa juu ya jengo refu kwa kuigiliza scene ya filamu ya King Kong alipokuwa amepanda kwenye jengo refu la New York la Empire State.
Picha hiyo iliyochorwa na mchora katuni Valerio Marini inaashiria jinsi Balotelli alivyoitawala Uingereza.
Hata hivyo maelfu ya wasomaji wenye hasira wameilaani picha hicho kwa kuonesha ubaguzi wa rangi dhidi ya Balotelli, ambaye wazazi wake walizaliwa nchini Ghana, na hivyo Gazzetta kulazimika kuomba radhi.
Gazeti hilo la mjini Milan limekiri kwa kusema: “Tunahitaji uangalifu zaidi na tahadhali.”
Balotelli ni mshambualiji wa Manchester City ya Uingereza na pia mchezaji wa timu ya taifa ya Italia.

                             SOURCE BONGO 5

TASWIRA MBALIMBALI ZA WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA BUNGENI MJINI DODOMA


 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na  Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza kwenye viwanja vya bunge Mjini Dodoma  Juni 26, 2012
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Moshi Mjini Philemon Ndesamburo (kushoto ) na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni Juni 26,2012.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Viti Maalum, Riziki Lulida (katikati) na Mbunge wa Mchinga,Said Mtanda kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 26,2012.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

Kituo cha afya chakatiwa umeme, wajawazito wajifungua na chemli


 Baadhi ya majengo ya Kituo cha Afya kilichopo Kata ya Songwa, Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga kama linavyoonekana pichani
Ofisa Tabibu wa Kituo cha Afya Songwa, Bundala Nandule
 KITUO cha Afya kilichopo Kata ya Songwa, Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga kimekatiwa umeme kwa takribani miezi saba sasa kikidaiwa bili ya umeme na TANESCO ya jumla ya sh. 38,000 hali inayowabebesha mzigo wa gharama wananchi wanaofika kupata huduma kituoni hapo.

Wagonjwa wanautibiwa usiku katika kituo hicho hasa wanawake wajawazito wanalazimika kugharamia mafuta ya taa kwenye chemli za kituo au kuchangia sh. 1200 kabla ya huduma yoyoto ili kupatikana mwanga unaowawezesha wahudumu kufanya kazi zao usiku.

Akizungumza na Thehabari.com juzi kijijini Songwa, Jamila Nyalulu mkazi wa eneo hilo alisema wananchi wasio na uwezo wa kuchangia mafuta ya taa hasa kwa huduma za uzazi wamekuwa wakipata tabu, jambo ambalo limekuwa likihatarisha maisha yao kiafya.

Ofisa Tabibu wa Kituo hicho, Bundala Nandule amekiri hali hiyo inakwamisha ufanisi wa utoaji huduma za afya hasa kwa wagonjwa wa usiku au wanaopumzishwa na kuongeza kuwa tarari wameripoti suala hilo katika uongozi wa Halmashauri ya Kishapu lakini bado linafanyiwa kazi.

“Tatizo la umeme linatusumbua kwa kweli hasa mgonjwa anapokuja kupata huduma usiku. Wagonjwa wa kawaida hulazimika kuja na tochi, lakini kwa wajawazito wanatakiwa kuja na fanta moja (chupa ya soda) ya mafuta ya taa au aje na sh. 1200 kwa ajili ya ununuzi wa mafuta hayo kabla ya huduma,” alisema Nandule.

Hata hivyo akizungumzia tatizo hilo, Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Kishapu, Lucas Said alisema wanamshangaa Mkuu wa Kituo hicho cha afya kushindwa kufuatilia malipo ya bili katika ofisi za halmashauri kwani cheki ya malipo ya bili hiyo iliandikwa tangu mwaka jana (2011).

“Kituo hicho kilikuwa kinadaiwa sh. 38,000 na cheki iliandikwa tangu mwaka jana lakini wahusika hawajatokea ili wakabidhiwe cheki hiyo…huu ni uzembe,” alisema kiongozi huyo wa Halmashauri ya Kishapu.

Kituo cha afya cha Songwa kinatoa huduma kwa zaidi ya vijiji vitatu vya Wilaya ya Kishapu, ambavyo ni pamoja na Kijiji cha Songwa, Bushola, Seseko na baadhi ya zahanati zilizopo jirani na kituo hicho.

*Habari hii imeandaliwa na Mtandao wa Thehabari.com (www.thehabari.com) kwa kushirikiana na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP).

SIMBA YAMTEMA RASMI JUMA JABU, HARUNA ATOLEWA KWA MKOPO

Juma Jabu
KLABU tano za Ligi Kuu ya Tanzania zimewasilisha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) majina ya wachezaji ambao zimewakatishia mikataba/mikataba yao kumalizika au kuwaacha kwa ajili ya usajili wa wachezaji msimu wa 2012/2013.
Kwa mujibu wa klabu hizo, wachezaji waliomaliza mikataba Simba kwa mujibu wa klabu hiyo ni Ally Mustafa, Derick Walulya, Gervais Kago, Juma Jabu wakati Salum Kanoni mkataba wake unatarajia kumalizika Juni 30 mwaka huu, wakati wachezaji ambao inakusudia kuwatoa kwa mkopo ni Rajab Isihaka, Salum Machaku, Haruna Shamte na Shija Mkina. 
Polisi Morogoro iliyopanda msimu huu imeacha wachezaji 17 wakati Tanzania Prisons ambayo pia imepata hadhi ya Ligi Msimu huu imeacha wachezaji 11. Azam imekatisha mikataba ya wachezaji watatu.
Wachezaji 12 wamemaliza mikataba yao katika klabu ya Kagera Sugar wakati wakati kwa upande wa Simba wachezaji waliomaliza mikataba ni wanne huku ikionesha nia ya kuwatoa kwa mkopo wengine wanne.
Uhamisho wa wachezaji kwa msimu huu ulianza Juni 15 mwaka huu na utamalizika Julai 30 mwaka huu wakati kipindi cha kuanza wachezaji (kwa wasio wa Ligi Kuu) ni kati ya Juni 15 na 30 mwaka huu.

Madhara ya Mgomo Wa Madaktari Tanzania..


                                  Hii ni wodi ya wamama wajawazito Sekou Toure
                            Nani alaumiwe kwa hali hii...
 Mgomo wa madaktari katika hospitali za serikali nchini umeingia siku ya tano huku Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi ikimwamuru Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Namala Mkopi, awatangazie madaktari hao wasitishe mara moja mgomo huo.

Jaji wa Mahakama hiyo, Lusekela Moshi, ametoa amri hiyo jana na kueleza kuwa Rais wa MAT anatakiwa kuwatangizia madaktari kupitia vyombo vya habari wasitishe mgomo huo hadi Julai 24, mwaka huu siku ambayo kesi ya madaktari itakaposikilizwa na kutolewa maamuzi.
 Alisema jalada linalowataka madaktari kusitisha mgomo tayari limekwisha kupelekwa kwa Rais wa MAT Jumatatu wiki hii na kwamba kinachosubiri ni rais huyo kuwajulisha wananchama hao wasikaidi amri ya mahakama.

Jaji Moshi alisema mahakama inamtambua Rais wa MAT kuhusika katika mgomo huo kwa sababu awali alisikika akizungumza na vyombo vya habari kwamba madaktari watagoma.

Kiongozi wa Mgomo wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana,angalia picha hapa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnTPhFKGzBmmmtW76I_91Zq3hDy9f2DY55umu0xvHX2voTCzpl7wt1D-mWohJSbNJNcmbAqJzcolWMqHHwkvLzCKMxokMQXNBHZfW6S9JFxjkpDUg0XS9GHxn8jNE_JmFsTf-gwwUDNS74/s1600/318043_495673313780425_200233519_n.jpg 


Kwa mujibu wa mtandao wa Jamii Forums Dr. Ulimboka ametekwa majira ya saa sita usiku na watu watatu waliokuwa na silaha za moto na kumpeleka kusikojulikana! Inasemekana alipigiwa simu na jamaa mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la 'Abeid' ambaye tangu mwanzo amekuwa akiwasiliana naye na kujiita afisa wa serikali na kudai kuwa alitaka aonane naye face to face kwa ajili ya mazungumzo.

Dokta huyo aliokotwa akiwa na hali mbaya sana na hawezi kuzungumza.

Tukio hilo limetokea wakati kumekuwepo na mgomo wa madaktari nchi nzima ambao hata hivyo wameonekana kusalitiana kwa kutokuwa na msimamo wa pamoja, kwani maeneo mengine yote huduma zimeendelea kama kawaida, isipokuwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Madaktari hao wametangaza mgomo usio na kikomo kwa lengo la kuishinikiza serikali kutimiza mahitaji yao, ikiwemo kuboresha mazingira ya kufanyia kazi pamoja na kuwapandishia mishahara.

Licha ya mgomo huo kuanza kuleta madhara kwa wagonjwa katika siku ya kwanza juzi, kwa madaktari kutofanya kazi katika hospitali mbalimbali nchini, jana hali hiyo ilikuwa tofauti kwani sehemu nyingi huduma ziliendelea kutolewa kama kawaida.
SOURCE THIS DAY MAGAZINE