Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, August 19, 2013

MAMA SALMA KIKWETE APOKEA TUZO MAALUM TOKA TAASISI YA BEN TV DIPLOMATIC AWARDS 2012.

IMG_9987Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akimsikiliza kwa makini Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Dkt.Fenella Mukangara wakati akitoa maelezo mafupi kuhusiana na tuzo ya Ben TV Diplomatic Awards-2012 aliyopewa dhamana na Taasisi ya Bright Entertainment Network (BEN) ya Uingereza ya kumkabidhi Mama Salma Kikwete Tuzo hiyo katika jitihada zake za kuendeleza rasilimali watu katika Taifa kwa mwaka 2012.
IMG_0004Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara akimkabidhi Tuzo ya Ben TV Diplomatic Awards-2012  Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ofisini kwake tarehe 19.8.2013. Tuzo hiyo ilitolewa kwa Mama Salma baada ya kuibuka mshindi miongoni mwa mataifa ya bara la Afrika, Caribean, Asia na Pacific kutokana na kazi za kuendeleza rasilimai watu hapa Tanzania.
IMG_0028Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akitoa hotuba fupi ya kushukuru mara tu baada ya kupokea Tuzo kutoka kwa Taasisi ya Bright Entertainment Network ya Uingereza iliyokabidhiwa kwake na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Fenella Mukangara tarehe 19.8.2013.IMG_0052IMG_0087Mke wa Rais na Mshindi wa Tuzo ya BEN TV DIPLOMATIC AWARDS-2012 Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara na baadhi ya wajumbe wa bodi ya WAMA, Mheshimiwa Zakhia Meghji, Makamu Mwenyekiti (kulia) na Mama Hulda Kibacha, Mjumbe wa bodi (kushoto).mara tu baada ya kupokea Tuzo hiyo ofisini kwake tarehe 19.8.2013.
PICHA NA JOHN LUKUWI 

No comments:

Post a Comment