![]()
Chege amepata ajali maeneo ya Temeke Jana 16 July mida ya saa nne usiku. Ajali imesababishwa na mwendesha pikipiki ambaye alikuwa amelewa sana na ameiba pikipiki alio kuwa anaendesha.Mwenye pikipiki alifika hospitalini na kusema alikuwa akijitayarisha kuwasha pikipiki yake huku akiva koti kwa ajili ya kujizuia na baridi ndipo alipo sukumwa pembeni na mlevi huyo na kuibiwa pikipiki yake . Kwa mwendo wa kasi sana pikipiki hio iliingia barabarani bila kujali magari wala usalama.
Chege amepata maumivu makali kwenye mkono wake wa kushoto na ameshapata matibabu hospitali ya Kinondoni mida ya saa sita usiku.
Kabla ya ajali chege alikuwa studio akitayarisha CD Ya show atakayo kwenda kufanya Kigoma pamoja na kigoma All star tarehe 17 July 2012. Baada ya kutayarisha hio CD Alikuwa aje kinondoni kujitayarisha na safari yake ya Kigoma mapema asubuhi.
Rais Samia: Mahakama Huru ni Nguzo ya Utawala Bora na Maendeleo ya Taifa.
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
amesema hakuna taifa linaloweza kufikia maendeleo endelevu na ustawi wa
wananchi w...
2 hours ago




No comments:
Post a Comment