Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, July 25, 2014

PICHA ZA AJALI YA FUSO ILIYOUWA WATU WATATU NA MAJERHU ZAIDI YA 47

UMATI WA WAKAZI WA KIJIJI CHA UCHUNGA WAKITAZAMA AJALI YA FUSO
Watu 3 wamekufa na wengine zaidi ya 47 wamejeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kwenda mnadani kupinduka wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga.

New Music: Dereva Makini-Barnaba, Amini, Dayna & Mr.Blue‏

IMG-20140725-WA0006 
Katika kuunga mkono jitihada za kupunguza ajali barabarani wakali katika muziki wa bongo fleva Mr Blue, Amini, Banaba Boy na Dyna Nyange wamerekodi wimbo wa pamoja kuhamasisha uzingatiaji wa usalama barabarani na kwenye vyombo vya usafiri. Wimbo unaitwa Dereva Makini umetayarishwa na katika studio za C9. Kampeni hiyo ya dereva makini imeandaliwa na Transevents Marketing ambao ndio wamiliki wa tovuti ya Kariakoo Digital kwa lengo la kutoa hamasa kwa madereva kuwa makini wanapoendesha magari ili kuwawezesha abiria kufika salama waendako.

MKUTANO KATI YA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM NA WANAMTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA NA TAMWA

 Usu Millya Mwanamtandao wa Ulingo wa Katiba na wanawake ambaye alikuwa ndiye mwezeshaji wa Mkutano huo ambao  ulikuwa ni wa siku mbili akiendelea kutoa mwongozo wa mkutano huo.
 Doreen E. Maro kutoka TAMPRODA ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba akiwakilisha Wafugaji Akileta Mrejesho wa walichokuwa wakikijadili katika Kundi lao juu ya mapendekezo ya kuimarisha Masuala muhimu ya Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya

TAZAMA PICHA ZA MABAKI YA NDEGE YA AIR ALGERIE ILIYODONDOKA YAPATIKNA


Abiria wote wa ndege ya Air Algerie waliangamia jangwani
Abiria wote na wahudumu wa ndege ya Air Algerie AH5017 waliangamia jangwani.
Rais wa Ufaransa Francois Hollande ametangaza kuwa majeshi ya ufaransa yamefaulu kupata mabaki ya ndege lakini hawakuweza kuokoa nafsi hata moja.
Aidha rais Francois Hollande ametangaza kuwa majeshi hao wamepata mtambo wa kunukuu sauti ''Blackbox'' huko Mali ilikoanguka ndege hiyo iliyokuwa ikielekea mji mkuu wa Algeria Algiers.

CHIKAWE AMSHUKURU RAIS KIKWETE KWA KUZINDUA MRADI WA MAJI NACHINGWEA


Rais Jakaya Kikwete (katikati) akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Mradi mkubwa wa Maji kwa upande wa Wilaya ya Nachingwea katika Kijiji cha Chiumbati mkoani Lindi. Mradi huo mkubwa wenye thamani ya Shilingi Bilioni 34.6 pia unajumlisha Wilaya ya Masasi iliyopo Mkoa wa Mtwara. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe. Wapili kushoto ni Waziri wa Maji, Prof Jumanne Magembe, na kushoto ni Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete.
Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chiumbati wilayani Nachingwea baada ya kuzindua Mradi Mkubwa wa Maji kwa

HAWA NI MIONGONI MWA WANAWAKE 10 BORA AMBAO WAMEONYESHA HARAKATI ZA MAENDELEO HAPA TANZANIA



UPO msemo uliotawala vichwa vya watu tangu dahari kwamba wanawake ni tabaka la kukaa nyumbani na kufanya kazi za ndani. Wao jukumu lao ni kumfurahisha mume na lingine ni kuwaandaa watoto kwa ajili ya kwenda shule na kufuatilia nyenendo zao darasani.

Miss Tanzania aliyechukua taji hilo mwaka 2001, Happiness Magesse ndiye aliyefanikiwa zaidi kimataifa kuliko wote, japo wapo wengine wanaojitahidi. Hivi sasa Happiness ‘Millen’ ni mwanamitindo wa kimataifa.
Happiness Magesse.
Ilivyozoeleka ni kwamba wanawake ni goigoi. Utaona bungeni kuna wabunge wa viti maalum ambavyo wengi hutafsiri kuwa ni vya upendeleo. Kwa maana kwamba uwezo wao kushindana kwenye majimbo na kushinda ni mdogo ndiyo maana wanapewa hivyo maalum kwao.

Katika mitihani, kuna unafuu wa alama za ufaulu kwa wanafunzi wa kike. Yaani wanaonekana hawana uwezo wa kushindana na wavulana. Vijijini, wanawake wamekuwa wakitumika kama nyenzo ya kilimo, yaani mama akalime ndiyo alishe familia, baba akacheze bao au kunywa pombe.

Miaka inakwenda, wapo wanawake wengi ambao wameweza kudhihirisha kwamba inawezekana kwa jinsi ya kike kuanzisha kazi na kufanikiwa. Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro ni mfano wenye nguvu kwa wanawake kufanikiwa.

Spika wa Bunge, Anne Makinda, Mchungaji Getrude Rwakatare na wengineo, ni kichocheo kinachotoa uthibitisho kuwa wanawake wanaweza. Ni suala la kuwaamini na kuwapa nafasi, kwa hakika wanaweza kufanya mambo makubwa mno.

Ukiachana na hao, ipo orodha ya wanawake vijana 10 ambao wanastahili pongezi. Wamepambana katika maeneo yao kiasi cha kupata mafanikio ambayo yameonesha njia. Inabidi tuwatambue na kuthamini jitihada zao kwa maana wameendelea kuthibitisha ndivyo sivyo kwa wale waliokuwa wanaamini kuwa wanawake si lolote kwenye utafutaji.
FLAVIANA MATATA

Mwaka 2007 alipokwenda kushiriki mashindano ya dunia ya Miss Universe na kushika nafasi ya sita, wengi walidhani huo ndiyo mwisho wake. Ilionekana hivyo kwa sababu warembo wengi wameshiriki mashindano ya dunia na baada ya kurudi nchini, hawakusikika tena.

PICHA ZA MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA LEO 25 JULAI, 2014

PIX 9.
PIX 1.

DAWASCO WAONDOKA NA VIFAA VYOTE VYA MWENYE KIWANDA CHA KUFYATUA MATOFALI KIMARA ALIYEKAMATWA AKIIBA MAJI

 Wafanyakazi wa kampuni ya Majembe Auction Mart wakifungua mashine ya kutengenezea matofali katika eneo la Kwa Msuguri, Kimara jijini Dar es Salaam.Wizara ya Maji iliamrisha kukamatwa kwa vifaa na mali mbalimbali za Martin Kessy aliyekuwa amejiunganishia maji kinyume na sheria na kufanya biashara ya kufyatua matofali.  Zoezi hilo linaendelea. Zoezi hilo limefanyika jana katika eneo la Kwa Msuguri, Kimara jijini Dar es Salaam jana.  .
 Mwenyekiti wa kamati maalum ya Wizara ya Maji, Eng. Hamis Blangson (kulia) akisikiliza jambo wakati

Mnigeria aliebeba dawa za kulevya alivyokamatwa Nairobi baada ya rubani kuugua.

 Mwanamume mmoja Raia wa Nigeria imebidi alazwe kwenye hospitali ya taifa ya Kenyatta Nairobi Kenya baada ya kugundulika alikua na mzigo wa dawa za kulevya wa vidonge 57 tumboni mwake.Huyu jamaa alikua anazisafirisha hizi dawa kutoka Lagos kwenda Bangkok lakini ghafla akaanza kupata maumivu baada ya kuchelewa kufikisha mzigo aloubeba tumboni mwake baada ya ndege waliyokua wakisafiria kutua Nairobi kwa dharura.Ilitua kwa dharura baada ya rubani kuumwa ghafla hivyo kulazimu ndege kutua Nairobi kisha abiria wote kupelekwa hotelini na hapo ndio Mnigeria huyu akaanza kuhisi maumivu makali tumboni.


Simon Ithae ambae ni mkuu wa mawasiliano hospitali ya Kenyatta amesema ‘alitueleza amemeza vidonge na alikua akiamini ndicho chanzo cha maumivu hivyo alipoona hawezi kustahamili aliita Polisi akidai

Rubani wa miaka 17 alietangaza kupaa na ndege nchi 15 amepata ajali na kufariki

 Ilikua taarifa kubwa sana pale mtoto rubani mwenye umri wa miaka 17 alipotangaza maamuzi ya kusafiri na ndege ndogo ya injini moja kwenye nchi mbalimbali duniani ikiwa ni ndani ya Mabara matano, vituo 25 ndani ya nchi 15 kwenye siku 30.Haris Suleman na baba yake mzazi ambae pia ni Rubani walichukua mafunzo mbalimbali ya kutua kwenye maji wakati wa dharura kabla ya kuanza safari yao waliyoiandaa kwa miezi wakiwa na lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya watoto wa familia masikini nchini Pakistan waweze kwenda shule.
Sasa imethibitika kwamba mtoto huyu rubani aliekua anataka kuweka rekodi ya dunia kwa kuwa rubani mdogo aliesafiri umbali mrefu, amefariki dunia na mwili wake kupatikana baada ya ajali ya ndege hiyo iliyotokea baharini Jumanne usiku ambapo Baba yake ambae walikua pamoja hajulikani alipo
 Marehemu Haris katikati wakati akizungumzia maandalizi ya safari hiyo.

MAGUFULI AKAGUA DARAJA LA NANGOO PAMOJA NA UJENZI WA BARABARA YA NDUNDU -SOMANGA, AMPA MKANDARASI MIEZI MIWILI KUIKAMILISHA

 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma mkoani Mtwara kabla ya Ufunguzi wa Barabara ya Masasi –Mangaka na uwekaji wa jiwe la msingi wa barabara ya Mangaka –Mtambaswala 71.5km
 Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli wakwanza kulia akipita juu ya daraja la Nangoo Wilayani Masasi wakati wa ukaguzi huku akifatiwa na  Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale, Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mhandis Mussa Iyombe pamoja na Mwakilishi kutoka  Benki ya Maendeleo ya Africa (ADB) Bi Tonia Kandiero.



 Sehemu ya barabara ya Ndundu Somanga kama inavyooneka baada ya mkandarasi kuanza kufanya kazi kwa kasi tofauti na hapo awali

AISHA BUI AMPA SIFA ZA KUTOSHA MSANII "GABO ZIGAMBA" KWA UMAHIRI WAKE WA KUIGIZA




Aisha bui amkubali Gabo kuliko msanii yoyote wa kiume anasema huyu ni msanii wa kipekee sana kwani anavaa uhusika wowote kwa wakati wowote 

MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAR 25.07.2014 VICHWA VIKUBWA MAPYA YAIBUKA UTUPAJI WA VIUNGO,VIGOGO UKAWA WAINGIA MITINI NA SIRI YA MTOTO ALIYEIBWA DAR YAFICHUKA

 

ELIMU DUNI NA ISIYO SAHIHI YA MATUMIZI YA KONDOMU INACHANGIA MAAMBUKIZI MAPYA YA VVU KWA VIJANA

DSC_0084
Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias akizungumza na washauri wa Vikundi vya Vijana wasikilizaji juu ya masuala muhimu kuhusiana na kuzuia maambukizi ya VVU na Afya ya Uzazi kwa Vijana wenye umri kati ya miaka 15-24 katika warsha ya kuwajengea uwezo washiriki hao katika matumizi ya mwongozo wa ufuatiliaji wa vipindi kwa wasikilizaji walengwa wa Mradi wa SHUGA Redio inayofanyika kwenye kituo cha Redio Nuru FM mjini Iringa.(Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog).
Na Mwandishi wetu
Tafiti zimebaini kwamba Vijana hawatumii Kondomu na hutoa sababu nyingi ikiwa ni pamoja na kutopata ladha wakati wa tendo la ndoa na kwamba inapunguza nguvu na visingizio vingine vingi vinavyopelekea kuashiria hatari ya maambukizi.
Hayo yameelezwa na Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias wakati akizungumza na washauri wa Vikundi vya Vijana wasikilizaji juu ya masuala muhimu kuhusiana na kuzuia maambukizi ya VVU na Afya ya Uzazi kwa Vijana wenye umri kati ya miaka 15-24 katika warsha ya kuwajengea uwezo washiriki hao katika matumizi ya mwongozo wa ufuatiliaji wa vipindi kwa wasikilizaji walengwa wa Mradi wa SHUGA Redio.
“Asilimia 40 ya Wasichana na Asilimia 47 ya Wavulana ndio wenye ufahamu wa kina juu ya maambukizi ya VVU huku asilimia kubwa wakiwa hawana elimu ya kutosha na hawajui afya zao kwa kuwa hawana utamaduni wa kupima VVU ”, amesema Bw. Mathias.
DSC_0184
Mkufunzi wa warsha hiyo Meneja Mawasiliano kutoka Pangani FM, Bw. Abdullah Mfuruki akiwapiga msasa washauri wa Vikundi vya Vijana kwenye warsha ya siku mbili inayoendelea mjini Iringa.

TUJUMUIKE PAMOJA LEO KUCHEZA WIMBO MPYA WA SKYLIGHT BAND "PASUA TWENDE" KIOTA CHA MARAHA THAI VILLAGE JIJINI DAR


Na hii ndio Video ya Skylight Band ya Wimbo mpya "PASUA TWENDE"

DSC_0078
Mary Lucos akitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band (hawapo pichani) huku akipewa sapoti na Hashim Donode sambamba na Digna Mbepera Ijumaa iliypoita kwenye viunga vya Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0099
Vijana wa Skylight Band wakijimwaga na sebene, kutoka kushoto ni Joniko Flower, Sony Masamba na Sam Mapenzi.
DSC_0102
Sio kwamba wanaanguka la hasha ni mbewembwe za Majembe ya Skylight Band katika kutoa burudani kwa mashabiki wao.
DSC_0118
Mdau aliguswa na uchezaji wa wanamuziki wa Skylight Band na kuchomoa bulungutu la mapesa na kuwatunza wote watatu kama inavyoonekana pichani.

BAADA YA KIMYA KIREFU HUU NDIO WIMBO MPYA WA ALI KIBA UITWAO MWANA,DOWNLOAD NA SIKILIZA HAPA

TAZAMA PICHA::FRANK LAMPARD ATUA RASMI NEW YORK CITY,ASAIN MIAKA 2


Smiles better: Frank Lampard was in chipper mood as he was officially confirmed as a New York City player


Welcome to the USA: Frank Lampard was officially unveiled as a New York City FC player on Thursday
Frank Lampard has completed his move to MLS side New York City FC after he was unveiled on Thursday.
The 36-year-old left Chelsea at the end of last season after 13 seasons and a club record 211 goals.
The midfielder becomes New York City FC's fourth player and second major summer signing following the arrival of David Villa from Atletico Madrid.


Touch down: Frank Lampard was pictured at JFK Airport on Wednesday evening ahead of today's unveiling

SERIKALI YAPOKEA MABEHEWA 25 YENYE THAMANI YA SH.BILIONI 4.3 KUTOKA INDIA

 Waziri wa Uchukuzi Dk.Harrison Mwakyembe (kulia), akiangalia moja ya mabehewa kati ya mabehewa 25 mapya ya kubebea kokoto yenye thamani ya sh.bilioni 4.3 aliyoyapokea kutoka Kampuni ya M/S Hindusthan Engineering and Industriles Limited ya India Dar es Salaam Leo, kwa ajili ya Kampuni ya Reli Tanzania (TRL). Wa pili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TRL, Mhandisi Kipalo Kisamfu.
 Waziri wa Uchukuzi Dk.Harrison Mwakyembe (katikati), akifurahia jambo wakati wa kupokea mabehewa hayo. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TRL, Mhandisi Kipalo Kisamfu na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk.Shaaban Mwinjaka.
 Mkurugenzi Mkuu wa TRL, Mhandisi Kipalo Kisamfu (mwenye tai kushoto),akimuelekeza jambo Waziri Mwakyembe.

MKURUGENZI WA THE GUARDIAN NA MHARIRI WA NIPASHE, WAITWA POLISI JIONEE HAPA

Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, (ZCO), Jafar Ibrahim, (Kulia), akizungumza na Mwanasheria wa kampuni ya The Guardian, Gladis Frimbari (Wapili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa The Guardian, Kiondo Mshana, (Wa pili kushoto) na Mhariri Mtendaji wa Nipashe, Jesse Kwayu, (Wa kwanza kushoto), ofisini kwake jijini. Kachero huyo aliwaomba radhi viongozi hao wa The Guardian, kutokana na makosa ya kuwaita polisi kwa mahojiano kuhusiana na habari iliyochapishwa na Nipashe ikiwahusisha polisi wa pikipiki na vitendo vya rushwa, na kwamba Polisi haina tatizo na habari hiyo. (Picha kwa Hisani ya The Guardian)
Mkurugenzi Mtendaji wa The Guardian Limited, Kiondo Mshana, (Katikati), Mhariri Mtendaji wa Nipashe, Jesse Kwayu, wakiwa kwenye Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Makosa ya Jinai, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, ZCO, Jafar Ibrahim jijini. Hata hivyo 

SERIKALI YASAINI MIKATABA MIWILI YA UJENZI WA BARABARA ZA JUU KWA JUU


1 (4)Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Masaki Okada (kulia) wakibadilishana hati ya makubaliano ya mikataba miwili ya ujenzi wa barabara za juu kwa juu katika makutano ya TAZARA na usambazaji umeme jijini Dar es salaam leo zenye thamani ya zaidi ya bilioni 128.
2 (4)Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (kushoto) na Balozi wa Japan nchini Masaki Okada (kulia) wakisaini hati ya makubaliano ya mikataba miwili ya ujenzi wa barabara za juu kwa juu katika makutano ya TAZARA na usambazaji umeme jijini Dar es salaam leo zenye thamani ya zaidi ya bilioni 128.


Mwanamke raia wa Sudan aliyesamehewa adhabu ya kifo baada ya kubadili dini amesafirishwa hadi nchini Italia Na Kuonana Na Papa


Mwanamke raia wa Sudan aliyesamehewa adhabu ya kifo baada ya kubadili dini amesafirishwa hadi nchini Italia baada ya kuwa kwenye ubalozi wa Marekani mjini Khartoum kwa zaidi ya mwezi mmoja.

Meriam Yahia Ibrahim Ishag na familia yake waliondoka na ndege ya serikali ya Italia wakiongozana na Waziri wa nchini Italia Lapo Pistelli.Baada ya kuwasili Italia bi Merian alikutana na Papa Francis ambaye alimsifu kwa kusimamia dini ya ukristu licha ya tishio la mauti.

Merian alikutana na papa katika makao yake rasmi ya Santa Marta iliyoko kwenye makao makuu ya kanisa Katoloki ya Vatican.


Mkutano huo ulidumu kwa takriban nusu saa .

Baba wa Meriam ni muislamu na kwa Misingi ya sheria ya dini hiyo nchini Sudan Meriam pia 

TAARIFA::KLABU YA YANGA YAKANUSHA KUJITOA MICHUANO YA KAGAME

Klabu ya Young Africans haijajitoa kushiriki mashindano ya Kombe la Kagame chini Rwanda kama inavyoripotiwa na baadhi ya mitandao ya habari nchini na kusema taarifa hizo ni za uongo.

Katibu mkuu wa Yanga SC Bw Beno Njovu amesema

TAZAMA PICHA 4 ZA MASHABIKI WA ISRAEL NA PALESTINA WAKIZICHAPA UWANJANI,MECHI YAAIRISHWA


Mashambulizi: Waandamanaji walivamia uwanja na kuanzisha dhoruba ya kuwashambulia wachezaji wa  Maccabi Haifa


 Waandamanaji walivamia uwanja na kuanzisha dhoruba ya kuwashambulia wachezaji wa  Maccabi Haifa